Juni 10, 2012
Serikali ya Kenya imetilaiana saini na Shirika la Maendeleo la Ufaransa makubaliano ya mkopo wa shilingi bilioni 8.3 (dola milioni 98.1), radio ya Kenya Capital FM News iliripoti hapo Ijumaa (tarehe 8 Juni).
Fedha hizo zitapelekwa katika ujenzi wa laini la kutolea umeme wa volteji kubwa katika eneo kubwa la Nairobi. Waziri wa Fedha Njeru Githae alisema mradi huo utatoa uwezo wa ziada wa usambazaji umeme kutoka viwanda vipya vya umeme wa ardhini katika Olkaria na kiwanda kipya cha umeme wa upepo kitakachojengwa karibunikatika ZiwaTurkana.
Waziri Njeru Githae alisema mradi huo utasaidia kiwango cha mahitaji kinachoongezeka cha umeme. “Tunataka kuhakikisha kuwa watoto wetu watakaozaliwa miaka miwili kutoka sasa kuwa katika maisha yao, neno “giza tupu” wawe hawalijui,” alisema.
Balozi wa Ufaransa Etienne de Poncins alisema hii ni ya kipaumbele kwa maendeleo mijini na ya kitaifa, ikiwa na uwezo wa kuwa na athari za muda mrefu.
“Mpango huu utasaidia kukuza maendeleo ya kijamii na kiuchumi mjini Nairobi na nchini kote kwa jumla kwa kuwa na umeme wa kutosha kwa madhumuni ya kiusalama,” alisema. “Kwa muda mrefu, tunataka kujishughulisha na mradi wa kuuanganisha umeme na Ethiopia na Tanzania chini ya Ubia wa Umeme wa Afrika ya Mashariki.”
Polisi nchini Tanzania wamewakamata watu 90 siku moja baada ya maandamano ambapo mtu mmoja aliuaw...
Kenya ililiomba Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa siku ya Alhamisi (tarehe 23 Mei) kufutwa kw...
Rais Hassan Sheikh Mohamud wa Somalia aliongoza sherehe za maadhimisho ya miaka 50 ya kuanzishwa ...
Mawaziri wa mambo ya nje wa mataifa wanachama wa Shirika la Maendeleo la Pembe ya Afrika (IGAD) w...
Kiongozi wa jamii huko Zanzibar, Mohammad Omar Said, alishambuliwa kwa tindikali siku ya Alhamisi...
Mahakama moja ya Puntland imewahukumu kifo watu saba kwa mauaji ya ulamaa wa Kisomali, Abdulkadir...
Shirika la kimataifa la misaada la Global Partnership for Education (GPE) limetangaza msaada wa d...
Shirika la kimataifa la kuteteta haki za binadamu la Amnesty International limetoa wito kwa Kenya...
Makamu wa Rais wa Kenya William Ruto ameahidi adhabu kali zaidi kwa majangili katika mswada wa Sh...
Raisi wa Kenya Uhuru Kenyatta siku ya Alhamisi (tarehe 23 Mei) alitoa majina mawili ya mwisho ya ...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji