Waziri wa Mambo ya Ndani wa Somalia atarajia Umoja wa Kitaifa

Juni 10, 2012

  • 1 Maoni
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Waziri wa Mambo ya ndani wa Serikali ya Mpito ya Shirikisho ya Abdisalam Moallin Mohamud aliahidi katika mkutano wa hadhara hapo Jumapili (tarehe 10 Juni) kuwa amani itarejea Mogadishu, Mtandao wa habari wa Somalia wa Shabelle News uliripoti.

Akizungumza kwenye sherehe katika wilaya ya Howlwadaag ya Mogadishu, Mohamud alisema mipango iko njiani ya kuimarisha usalama, sheria na kanuni mjini.

“Ninawaomba watu wa Mogadishu kushirikiana pamoja na kuvisaidia vikosi vya usalama vya serikali ya Somalia kudhibiti usalama kwa jumla jijini ili kuzuwia mashambulizi na mauaji dhidi ya raia,” alisema.

Mwezi uliopita, mfulizo wa milipuko jijini iliua kiasi cha watu saba, wengi wao wakiwa askari. Wiki iliyopita watu wenye silaha walimuua mfanyabiashara mmoja wa Uturuki.

Mogadishu imekuwa katika udhibiti wa Serikali ya Mpito ya Shirikisho tangu al-Shabaab walipolazimishwa kuondoka mwezi Agosti 2011.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 1)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Maoni ya msomaji

  • Tumusiime Godwin
    June 12, 2012 @ 01:28:30PM

    Asanteni sana majeshi ya AMISOM (UA) kwa kazi mliyofanya; baada ya miaka 20 Somalia amani inaweza kurejeshwa sasa, na kwa kweli mnastahiki sifa kwa hilo. Maisha marefu AMISOM, maisha marefu kwa UA. Kwa upande wangu, sitaki mazungumzo ya amani na al-Shabaab kwa sababu wameshaona baada ya kushindwa ndio wanataka mazungumzo, hapana. AMISOM endeleeni na kuwafunza nidhamu al-Shabaab bila ya huruma.

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo

Nyenzo