Waandishi wa habari Somalia walaani kupigwa risasi mwandishi wa habari

Juni 10, 2012

  • 2 Maoni
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Waandishi wa habari na vikundi vya vyombo vya habari vimelaani mauaji yanayolengwa waandishi wa habari baada ya watu wenye silaha kumpiga risasi na kumjeruhi mtoa habari wa radio Mohamed Nur Sharif siku ya Ijumaa jioni (tarehe 8 Juni).

Sharif, anayefanyakazi katika Radio Bar-Kulan inayofadhiliwa na UN, alipigwa risasi alipokuwa akirejea nyumbani kutoka mitaa ya Hamar Jajab mjini Mogadishu. Watu watatu waliokuwa na bastola walimpiga risasi Sharif mara mbili, moja ya kifua nyengine ya mgongo, Bar-Kulan iliripoti.

Sharif alifanyiwa upasuaji anaendelea vizuri. Hii ni mara ya pili kwa Sharif kujeruhiwa akiwa kazini. Mwezzi wa Aprili, alikuwa miongoni mwa waandishi wa habari zaidi ya kumi waliojeruhiwa katika bomu la kujitoa muhanga la al-ShabaaJumba la Taifa la Maonesho

"Tunalaani mashambulizi haya ya kutisha dhidi ya wenzetu wakati washambuliaji hao hawaadhibiwi,” alisema Katibu Mkuu wa Umoja wa Kitaifa wa Waandishi wa Habari wa Somalia Mohamed Ibrahim. “Tunaitaka serikali ya Somalia kufanya uchunguzi huru mara moja kuhusu tukio hili.”

Jumuiya ya Waandishi wa Habari wa Somalia walioko Uhamishoni huko Nairobi (SEJASS) pia walilaani jaribio hilo la mauaji na kuitaka serikali ya Somalia “ kufanya uchunguzi wa kina wa kesi hii na kuwakamata washambuliaji waliohusika”.

“Mashambulizi dhidi ya waandishi wa habari kunahatarisha uhuru wa vyombo vya habari nchini,” mwenyekiti wa SEJAS Mohamed Osman Hussein alisema katika taarifa.

Hakuna kikundi kilichodai kuhusika na shambulio hilo. Mpaka sasa, waandishi wa habari watano wa Somali wameshauliwa mwaka huu na watu wenye silaha wasiojulikana.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Maoni ya msomaji

  • nagiib
    June 12, 2012 @ 08:34:31AM

    Kuna habari gani za karibuni kutoka Somalia?

  • John Mwangi
    June 11, 2012 @ 07:20:41AM

    Al-Shabaab waelewe kuwa wanajichimbia kaburi lao wenyewe. Wanajisafishia njia ya kujimaliza wenyewe kwa kuua watu wasio na hatia.

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, katiba ya Kenya inapaswa kurekebishwa ili kulipa baraza jipya la Seneti madaraka zaidi?

Angalia matokeo