Juni 10, 2012
Waziri wa Usalama wa Ndani wa Kenya George Saitoti (kulia) akizungumza na Katibu Mkuu wa UN BanKi-moon katika Uwanja wa Ndege wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi mwezi Machi 2011. [Simon Maina/AFP]
Saitoti, mwenye umri wa miaka 66, alikuwa mgombea wa urais katika uchaguzi ujao na mtu muhimu katika kuendesha mapambano ya Kenya dhidi ya kikundi cha al-Shabaab wanaoshirika na al-Qaida katika nchi jirani ya Somalia. AFP iliripoti.
Helkopta hiyo ilidondoka katika msitu wa Kibuku kama saa 2:30 hivi asubuhi, muda mfupi tu baada ya kunyanyuka kutoka uwanja wa ndege wa Wilson wa Nairobi. Ilikuwa ikielekea kwenye sherehe za kidini huko magharibi mwa Kenya. Manahodha wawili na mabodigadi wawili pia walifariki katika ajali hiyo ya kuanguka kwa helkopta.
Rais Mwai Kibaki alisema katika taarifa kuwa vifo hivyo ni pigo kubwa kwa nchi yetu”.
"Waziri Saitoti atakumbukwa siku zote kwa kuwa alikuwa mchapakazi na aliyetumikia utumishi wa umma akitumia muda wake kuhudumia watu wa Kenya,” Kibaki alisema.
“Serikali itahakikisha uchunguzi wa kina wa ajali hiyo” kilichosababisha kuanguka . Waziri Mkuu Raila Odinga aliwaambia waandishi wa habari katika eneo la tukio.
Baadhi ya wabunge wa Somalia wameitupilia mbali hoja ya kumtaka waziri mkuu na baraza lake la maw...
Wabunge wa upinzani walidai kwamba serikali ya Tanzania imekuwa ikibana uhuru wa kujieleza na kud...
Sampuli ya DNA iliyochukuliwa kwenye mswaki uliokuwemo kwenye begi lililokuwa na risasi lililopat...
Wakenya kumi na wasaba wameshtakiwa kwa kuvunja amani, kufanya ghasia na ukatili dhidi ya wanyama...
Al-Shabaab imedai kuhusika na urushwaji wa makombora kwenye kasri ya rais mjini Mogadishu siku ya...
Wanajeshi wa Uganda wa Kikosi Namba 9+ wanarudi nyumbani baada ya kukamilisha miezi 13 ya ziara y...
Kikosi cha polisi cha Kenya kitaanza uhakiki wa kina wa maofisa mwezi ujao, kikianza na kusaili w...
Ujambazi ulizuiwa katika ofisi za usalama za Wells Fargo huko Mombasa ulisababisha kifo cha watu ...
Rais wa Ghana John Dramani Mahama aliahidi msaada wa nchi yake katika kipindi cha ujenzi mpya wa ...
Polisi nchini Tanzania walimkamata mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msingwa, na wafanyabiashara 60 k...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji
Maoni ya msomaji
George Saitoti alikuwa mtu mkubwa, Daima atakumbukwa kwa msimamo wake thabiti dhidi ya utawala wa kidikteta wa Moi . Huko Kasarani na mbele ya Raisi Moi mtu huyu mzuri alisema, "zinakuja nyakati ambazo taifa litakuwa kubwa kuliko mtu binafsi." Huyu ndiye mtu ambaye alipaswa kuwa raisi wa nne wa jamhuri ya kenya. Roho yake na ya Msaidizi wake Ojodehh na wanne wengine ambao walikufa pamoja naye zipumzike katika amani ya milele. Dr Theuri Matthew Mwangi.
Ilikuwa inashitusha kupòkea habari mbaya kama hizo. hata hivyo hakuna tunachoweza kufanya isipokuwa kukubali kuwa tumepoteza. Ningependa tu kuwafariji wanafamilia na marafiki zake. Tumuombe Mungu awape amnai katika wakati huu mgumu. Wote wawili Mungu awalaze pema - Amen.
Waziri wa Usalama wa ndani Professor Goerge angekuwa Raisi ajaye wa Kenya siku za mbele kwa mujibu wa uchambuzi wangu. Daima hakuwakandamiza wanasiasa wengine. Alikuwa rafiki wa jumuiya ya Kisii pamoja na Kenya kwa jumla. Mungu ibariki familia yake.