Watu wa Somalia waliokimbia makazi yao wapewa nyumba mpya.

Juni 08, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Mamia ya watu wa ndani waliokimbia makazi yao huko Puntland walipewa nyumba mpya hapo Alhamisi (tarehe 7 Juni) wakati wa sherehe za makabidhiano iliyoongoza na baraza la Wakimbizi la Norwei (NRC) na Kamiheni ya Wakimbizi ya UN (UNHCR).

Mahirika ya wakimbizi yalitoa makazi 250 ya kudumu kwa jamii huko Kaskazini ya Galkayo, na kuwapatia makazi kwa watu 1,500 waliokimbia makazi yao, NCR ilisema.

Maafisa wa ndani na kimataifa walihudhuria sherehe hizo katika makazi ya Halaboqad, ambao walitoa hotuba na watoto kuimba. NCR na UNHCR waligharimia na kuendaa ujenzi wa nyumba hizo.

“Ni siku njema kushuhudia familia zote zinapata funguo za nyumba zao mpya,” alisema Hassan Khaire, mkurugenzi wa kanda ya NRC. “Watu hawa wamekuwa wakihamishwa mara kadhaa na wameteseka kwa miaka mingi ya mapambano. Kupata kwao makazi mapya kutawarahisishia kuanzisha upya maisha ya heshima.”

“Kwa kutoa ardhi na kuipatia kila familia cheti cha umiliki, Manispaa ya Galkayo ya Kakazini ilikuwa na njia ndefu ya kuwafanya watu waishi kwa maikilizano,” alisema Mwakilishi wa UNHCR nchini Somalia Bruno Geddo.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo