Serikali ya Somalia yakaribisha zawadi za Marekani juu ya viongozi wa al-Shabaab

Juni 08, 2012

  • 1 Maoni
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Serikali ya Mpito ya Shirikisho ya Somalia (TFG) hapo Ijumaa (tarehe 8 Juni) ilikaribisha zawadi ya mamilioni ya dola kama zawadi kwa habari zitakazopelekea kukamatwa kwa viongozi wa al-Shabaab.

“Tangazo kutoka serikali ya Marekani leo kuweka zawadi ya dau la dola milioni 7 kwa kiongozi wa kigaidi wa al-Shabaab bila shaka kutasaidia juhudi za serikali ya Somalia za kumaliza utawala wa vitisho wa al-Qaeda nchini Somalia,” TFG ilisema katika taarifa.

Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani iliwaongeza viongozi saba juu wa kikundi cha al-Shabaab chenye mafungamano na al-Qaeda kwa mpango wake wa Zawadi kwa ajili ya Haki hapo Alhamis.

Kiwango cha juu kabisa kilitolewa kwa muanzishaji wa kikundi, Ahmed Abdi aw-Mohamed, anayejulikana pia kama Ahmed Godane au Mukhtar Abu al-Zubair, kwa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani kutoa zawadi ya dola milioni za zawadi kwa habari za kujua alipo.

TFG ilisema Godane ni “dhamana wa mauaji ya wananchi wasio na hatia nchini Somalia, ikiwa ni pamoja na mfululizo wa mashambulizi ya kigaidi ambayo al-Shabaab wanafanya katika nchi za jirani.”

Dola nyingine milioni 5 zilitolewa kwa wanachama wengine wa al-Shabaab -- Ibrahim Haji Jama, Fuad Mohamed Khalaf, Bashir Mohamed Mahamoud na Mukhtar Robow.

Mpaka dola milioni 3 zilitolewa kwa Zakariya Ismail Ahmed Hersi na Abdullahi Yare.

“Hiki ni hali muhimu sana katika historia ya Somalia, ambapo uwezekano wa kupatikana tena nafuu upo karibu baada ya miaka mingi ya machafuko,” taarifa ilisema. “Serikali ya Somalia inatoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kuendelea kuzisaidia asasi ili kuhakikisha kuwa Somalia inashinda vita dhidi ya al-Qaeda, ambao wanashindwa kwa msaada wa watu wa Somalia.”

Uongozi wa Ahlu Sunna wal Jamaa katikati ya Somalia pia ulikaribia dau hilo la Marekani, na kuliita kuwa ni hatua moja mbele katika vita dhidi ya al-Shabaab, iliripoti Redio Bar-Kulan inayofadhiliwa na Umoja wa Matiafa.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 7)

Dislike_icon(1)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Maoni ya msomaji

  • أحمد عبد الرحيم
    June 9, 2012 @ 09:37:11PM

    Vikundi vya kigaidi vimepoteza wafuasi wao kwa sababu walikamatwa au kuuliwa wakati wa mapambano yaliyopinga vikosi vya usalama. Hii ndio sababu siku zote wanaandikisha wanachama wapya ili kuua watu wasio na hatia. Kwa hivyo, vyombo vya habari vinapaswa kufahamu wajibu wao, katika kuwaamsha vijana dhidi ya mbinu zao za kuwavutia. Pia mashule na vyuo vikuu vina nafasi muhimu, pamoja na misikiti na viongozi wa jamii ambao wana wajibu katika jamii ya Iraki. Wanapaswa kwenda mara moja, kuzuia uandikishwaji na kuwarubuni vijana. Kufanya hivi kutarejesha nyuma ugaidi. Watoto wetu wakiungana nao, majaliwa yao yatakuwa ni kifo katika mikono ya watu hawa wabaya na wahalifu; wanawatumia watoto wetu kwa kuwajaribu kwa pesa na madawa ya kulevya, au kuwadanganya kwa kutumia dini na kudai kuwa wanalinda watu na kwamba wako dhidi ya ugaidi. Kwa kweli, ni waongo, walaghai na wanavunja moyo; kwa hivyo hali halisi ya wahalifu na watu wabayahawa lazima ielezwe wazi.

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo