Mei 31, 2012
Mkuu wa jeshi la Kenya hapo Jumatano (tarehe 30 Mei) alisema kwamba AMISOM itauteka mji wa bandari wa Kismayo unaodhibitiwa na al-Shabaab ndani ya miezi mitatu.
Mji wa bandari wa Kismayo ni mji wa mwisho muhimu unaodhibitiwa na washirika wa al-Qaeda, al-Shabaaab, ambao katika miezi ya hivi karibuni wameanza kutumia mbinu za vita vya msituni wakati vikosi vya kanda vinaendelea kuwanyang'anya maeneo.
“Shabaha yetu hii itatokea kabla ya mwezi Agosti wakati utawala wa Serikali ya Mpito ya Shirikisho itakapomaliza muda wake,"alisema Jenerali Julius Karangi mjini Nairobi, kwa mujibu wa AFP. Vikosi kutoka Jeshi la Ulinzi la Kenya kwa sasa linafanya shughuli zake chini ya usimamizi wa AMISOM.
“Tunaendelea kutoa shinikizo kwa al-Shabaab,” Karangi alisema.
Wakati huo huo, majeshi ya Kenya yaliingia mji wa kusini ya Somalia wa Afmadow hapo Jumatano.
"Mji wa Afmadow unaanguka; bado kuna mapigano, lakini mpaka kumepambazuka utakuwa wetu,” alisema msemaji wa jeshi la Kenya Kanali Cyrus Oguna.
Wapiganaji wa al-Shabaab huko Afmadow, ambayo iko umbali wa kilomita 120 ndani ya Somalia kutoka mpaka wa Kenya, walizuia mashambulizi ya majeshi ya Kenya kwa miezi kadhaa, na kuyazuia yasisonge mbele kuelekea Kismayo.
Ujumbe kutoka Jumuiya ya Maendeleo ya Pembe ya Afrika (IGAD) uliwatembelea maafisa mjini Mogadish...
Mshukiwa wa ugaidi na mke wake walipigwa risasi na kufa na maafisa sita wa polisi walijeruhiwa wa...
Watu watano walikamatwa siku ya Jumanne mjini Dar es Salaam wakiwa na vifaa vya kulipua katika mi...
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta aliwataka wabunge kuweka kando madai yao ya kuongezwa mishahara kwa ...
Majeshi ya serikali ya Somalia waliwaua wanamgambo tisa wa al-Shabaab wakati wa mapambanao hapo J...
Mtu asiyejulikana alimpiga kwa risasi na kumuua ofisa wa kitengo cha usalama cha kijeshi huko kas...
Muungano wa Jubilee tawala cha Kenya kilichukua uongozi wa kamati mbili muhimu za bunge Ijumaa (t...
Chama cha Wafanyabiashara na Asasi ya Chakula na Kilimo ya Umoja wa Mataifa vinatoa mafunzo kwa w...
Balozi wa Umoja wa nchi za Ulaya nchini Tanzania Filiberto Ceriani Sebregondi aliwahamiza waandis...
Makamu wa Rais wa Kenya, William Ruto, alisema kazi za Misheni ya Umoja wa Afrika nchini Somalia ...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji
Maoni ya msomaji
Mimi si Muislamu, lakini furaha yangu ni ulimqengu wote kuishi kwa amani. Hakuna mtu atakayemuua mwengine kwa jina la dini, kwa sababu hayo si maumbile. Maumbile na Dini vinapaswa kukaa pamoja kwa dhamiri moja, kwa sababu kile kilicho kizuri hakihitaji kuelezwa. Somalia lazima iwe huru hatimaye kutoka mikono ya wahalifu hawa.
Maombi yetu sio kwa watu wetu tu bali pia kwa watu wa Somalia ambao wanashiriki katika kukombolewa kwa nchi. Mungu atapigana kwa ajili yenu. Ushindi utakuwa wenu.
Hilo litakuwa jambo zuri na tunawatakia kila la heri katika shughuli zenu zote. Mwenyezi Mungu awaongoze kama alivyomuongoza Daudu alipopambana dhidi ya Goliath.