Rais wa Somalia atoa wito kwa wakazi wa Afogye kushirikiana na serikali

Mei 30, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Rais wa Somalia Sharif Sheikh Ahmed na baraza la mawaziri walitembelea wilaya ya Afgoye mnamo Jumanne (tarehe 29 Mei) na walizungumza na wakazi wa eneo hilo lililokombolewa upya, Shirika la Habari la Taifa la Somalia liliripoti.

Rais huyo, ambaye alinusurika na majaribio ya mauaji siku hiyo, alitembelea Elasha Biyaha na Alamade na kuwahimiza wakazi kushirikiana na vikosi vya usalama na serikali ya Somalia. Ujumbe wake uliwajumuisha mawaziri, watunga sheria na maofisa waandamizi wa usalama.

Kamanda wa jeshi wa Somalia na vikosi vya AMISOM walimkaribisha rais huyo na ujumbe wake, wakiimarisha usalama katika eneo hilo, shirika hilo liliripoti.

Rais huyo alivishukuru vikosi vya Somalia na vya Umoja wa Afrika kwa ushindi wao dhidi ya al-Shabaab huko Afgoye.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo