Polisi ya Somalia yaonesha mwili wa mshukiwa wa al-Shabaab

Mei 24, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Polisi wa Somalia wameonesha mwili wa mshukiwa mpiganaji wa al-Shabaab aliyepigwa risasi wakati akiwa amebeba maguruneti ambayo polisi wanaamini kuwa yalitumike kwenye mashambulizi ya soko la Bakara, Mtandao wa Habari wa Shabelle nchini Somalia uliripoti siku ya Jumatano (tarehe 23 Mei)

"Alikuwa mmoja kati ya vijana wanaorubuniwa na kundi la al-Shabaab na vikosi vyetu vya polisi walimuua usiku uliopita kwenye soko hii baada ya kupewa taarifa zake na wenyeji," alisema Msemaji wa Polisi ya Somalia Abdullahi Hassan Barise. "Tunatoa wito kwa vijana waliojiunga na al-Shabaab kuachana na kundi hilo na kujutia yale wanayoyafanya dhidi ya nchi yao.”

Jeshi la Polisi nchini Somalia limekuwa likiendesha operesheni kubomoa biashara haramu kwenye mitaa mbalimbali kwenye soko la Bakara. Mwishoni mwa wiki iliyopita, washambuliaji wasiojulikana walirusha maguruneti dhidi ya askari waliokuwa wakivunja majengo yasiokuwa halali katika soko la Bakara na kuwaua wawili kati yao.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo

Nyenzo