Vikosi vya Somalia, AMISOM vyakaribia Afgoye

Mei 24, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Vikosi vya majeshi ya Somalia na wale wa Umoja wa Afrika (AMISOM) wanakaribia kwenye mji wa Afgoye unaodhibitiwa na wapiganaji wa al-Shabaab, alisema msemaji wa AMISOM hapo Jumatano (tarehe 23 Mei).

“Vikosi vinaaendelea vizuri na opresheni inakwenda kama ilivyopangwa,” alisema msemaji Luteni Kanali Paddy Ankunda aliiambia Mtandao wa habari wa Shabelle, akiongeza kusema kwamba hivi karibuni watachukua uongozi wa wilaya hiyo. Amesema vikosi visaidizi viko umbali wa kilometa 30 kaskazini magharibi mwa Mogadishu. Amewataka wakaazi wa eneo hilo kubakia majumbani mwao.

Vikosi vya washirika vimepiga "hatua nzuri", kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa na vikosi hivyo siku ya Jumatano.

Lengo la “Operesheni huru ya Shabelle” ni kuwapa ulinzi watu 400,000 wa eneo la Afgoye”, makaazi ya kundi kubwa la watu hao waliotawanyika kwa kiasi kikubwa duniani, ilisema taarifa hiyo.

Kamanda mwandamizi wa al-Shabaab na kikosi chake cha ulinzi waliuawa wakati wa mapigano ya siku ya Jumanne, ilisema taarifa hiyo.

"Operesheni hiyo imeendelea kufanya vizuri. Magaidi wa al-Shabaab wanakimbia,” alisema Luteni Jenerali Andrew Gutti. “Wanajua kuwa wanapoteza mwelekeo, na pia wanapoteza marafiki katika maeneo mbalimbali ya Somalia. Tunatoa wito kwa watu wa mji wa Afgoye kutoa sehemu za kigeni zinazobaki maeneo mwao.”

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 5)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo