Mahiga: al-Shabaab washindwa huko kusini na kati mwa Somlia

Mei 23, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Mjumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia Augustine Mahiga alitangaza Jumatano (tarehe 23 Mei) kuwa al-Qaeda walioshirikana na al-Shabaab wameshindwa katika mapambano huko Somalia ya Kusini na Kati.

Mahiga aliuambia mkutano wa Mpango Mkuu huko Addis Ababa kuwa jana mapambano ya AMISOM na TFG dhidi ya gome za al-Shabaab katika ushoroba wa Afogoye ilikuwa ishara ya kushindwa kwa al-Shabaab, akiongezea kuwa kundi hilo liko katika hali ya kukimbia, Mtandao wa Shabelle Media Network wa Somalia uliripoti.

Katika habari zinazohusiana na hizo, Jenerali wa Somalia Abdikarim Yusuf aliuambia mtandao wa Shabelle kuwa AMISOM na serikali ya Somalia wanafikiria kuongeza mashambulizi ya jeshi lao dhidi ya al-Shabaab na kuahidi kuwa watashambulia kundi hilo la wanamgambo popote walipo katika nchi hii. Yusuf alisema kuwa wapiganaji wa al-Shabaab wanakumbana na fursa zao za mwisho za kujisalimisha.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo