Wavuvi wa kigeni wa nyavu zakukokota wavua vivivyo halali katika bahari ya Puntland

Mei 22, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Vyombo viwili vya kigeni vinavyotumia nyavu za kukokota zinavua visivyo halali katika bahari ya Puntland, kuwepo kwao kunaiumiza sekta ya uvuvi kwa wenyeji, alisema meya wa wilaya ya Bayla hapo Jumatatu (tarehe 21 Mei).

“Jumapili usiku, vyombo hivyo vya kigeni vinavyotumia nyavu za kukokota vilionekana katika bahari ya Bayla,” Meya wa Bayla Saeed Adan Ali alisema, kwa mujibu wa Mtandao wa habari wa Garowe Online wa Somalia. “Vyombo hivi vinasababisha hasara kubwa kwa mwambao wetu na watu wake."

Meya alisema wavuvi wa kukokotoa wa kigeni wanaathiri upatikanaji riziki wa wavuvi wa eneo hili, kwa vile wanajaribu “kuvua kupita kiasi na kuharibu viumbe vya baharini, yote haya yakiwa na athari kubwa sana kwa wavuvi wetu".

Alisema viongozi wa eneo hawana vifaa vya kuwazuia wavuvi hao, ambao wanavua umbali wa maili mbili za baharini nje ya mwambao.

Nyavu za kukokota mara nyingi huharibu viumbe vya baharini, ikiwa ni pamoja na kamba wanaoishi karibu na sakafu ya bahari, vyombo vya habari vinaripoti.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 1)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, serikali za majimbo ya shirikisho ziundwe vipi nchini Somalia kufuatia utata wa Jubbaland?

Angalia matokeo