Mei 22, 2012
Zaidi ya wapiganaji 40 wa al-Shabaab huko Somalia ya Kati waliasi na kujisalimisha kwa vikosi vya serikali na Ahlu Sunna wal Jamaa, Shirika la Habari la Taifa la Somalia liliripoti Jumanne (tarehe 22 Mei).
Wengi wa wapiganaji hao wanatokea Galgadud, ambapo vikosi vya Serikali ya Mpito ya Shirikisho vipo katikati ya kampeni ya kuwaondoa al-Shabaab.
“Wapiganaji hawa walituita mwanzoni mwa mwezi Aprili na kutuomba msaada. Tuliwaahidi kuwasaidia kutoka katika kundi la al-Shabaab na tulifikia mwisho wa makubaliano yetu,” Kiongozi wa operesheni za jeshi la Ahlu Sunna wal Jamaa katika wilaya ya El Bur Abdi Hassan Mohamed aliliambia shirika rasmi la habari. “Tunawakaribisha, kwa kuwa ni watoto wetu ambao walioshauriwa vibaya.”
Wapiganaji hao walikataa ukatili na al-Shabaab dhidi ya raia wa Somalia.
Katika tukio tofauti, wapiganaji 10 wa al-Shabaab waliripotiwa kulihama kundi hilo na kujisalimisha kwa vikosi vya usalama katika mkoa wa Hiraan.
Waziri wa Ulinzi wa Somalia Hussein Arab Isse alisema kuwa mpiganaji yeyote wa al-Shabaab ambaye ataasi na kujiunga na serikali atapewa uangalizi kamili wa maisha.
Baadhi ya wabunge wa Somalia wameitupilia mbali hoja ya kumtaka waziri mkuu na baraza lake la maw...
Wabunge wa upinzani walidai kwamba serikali ya Tanzania imekuwa ikibana uhuru wa kujieleza na kud...
Sampuli ya DNA iliyochukuliwa kwenye mswaki uliokuwemo kwenye begi lililokuwa na risasi lililopat...
Wakenya kumi na wasaba wameshtakiwa kwa kuvunja amani, kufanya ghasia na ukatili dhidi ya wanyama...
Al-Shabaab imedai kuhusika na urushwaji wa makombora kwenye kasri ya rais mjini Mogadishu siku ya...
Wanajeshi wa Uganda wa Kikosi Namba 9+ wanarudi nyumbani baada ya kukamilisha miezi 13 ya ziara y...
Kikosi cha polisi cha Kenya kitaanza uhakiki wa kina wa maofisa mwezi ujao, kikianza na kusaili w...
Ujambazi ulizuiwa katika ofisi za usalama za Wells Fargo huko Mombasa ulisababisha kifo cha watu ...
Rais wa Ghana John Dramani Mahama aliahidi msaada wa nchi yake katika kipindi cha ujenzi mpya wa ...
Polisi nchini Tanzania walimkamata mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msingwa, na wafanyabiashara 60 k...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji
Maoni ya msomaji
Ni vyema kuwa wanamgambo wa al-Shabaab sasa wanatambua makosa yao baada ya nguvu kutumika. Hii inathibitisha imani yangu kuwa "ikiwa demokrasia imeshindwa, huna njia nyingine isipokuwa kutumia nguvu."