Polisi wa Kenya wamtafuta raia wa Kijerumani aliyeshirikana na al-Shabaab

Mei 18, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Polisi wa Kenya walisema Ijumaa (tarehe 18 Mei) kuwa wanamtafuta mwanaume wa Kijerumani wakitaka kumhoji kuhusu ushirikiano wa al-Shabaab wa Somalia waliowashirika na al-Qaeda.

Polisi wa Kenya mwishoni mwa wiki iliyopita walianza kumsaka Ahmed Khaled Mueller, aliyezaliwa Bonn, wakisema anaweza kuwa na taarifa kuhusu shughuli zilizopangwa na al-Shabaab.

Mnamo Jumatano, polisi walisema wamemkamata mwanaume ambaye wanaamini kuwa ni mshukiwa wa Kijerumani, lakini hawakuwa wamemtambua rasmi. Mwanaume huyo aligundulika kuwa raia wa Ujerumani lakini sio yule wanayemtafuta, alikamatwa kwa mashtaka ya dawa za kulevya, kwa mujibu wa AFP. Maofisa wa Polisi wa Kenya walisema msako wa Mueller unaendelea.

Kenya imekuwa ikikumbwa na mashambulio kadhaa toka ilipotuma vikosi kwenda Somalia ya kusini Oktoba 2011 kupambana na al-Shabaab.

Huko Mombasa, mlinzi wa usalama aliuawa na watu watano kujeruhiwa wakati mtu mwenye silaha alipofyatua risasi kwenye mgahawa wa Belle Vista Jumanne.

Polisi wa Kenya walitoa tahadhari kuwa Mueller anaweza kuwa na silaha na inaaminika pia anatumia majina ya Andreas Martin Muller na Abu Nusaibah.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 1)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, serikali za majimbo ya shirikisho ziundwe vipi nchini Somalia kufuatia utata wa Jubbaland?

Angalia matokeo