Mei 17, 2012
Vikosi vya usalama vya Serikali ya Mpito ya Shirikisho ya Somalia vinakaribia ngome ya al-Shabaab katika wilaya ya Hudur ya kusini mwa Somalia, mbunge wa Somalia Ahmed Sheikh Mohammed aliuambia mtandao wa Shabelle Media Network siku ya Alhamisi (tarehe 17 Mei).
Kama Mungu akipenda, tutachukua sehemu iliyobakia inayomilikiwa na waasi karibu na Hudur hivi punde kutoka kwa wapiganaji wa al-Shabaab,” Mohammed alisema. “Tuko umbali wa kadri ya kilometa 10 tu.”
Katika habari zinazohusiana na hizo, vikosi vya usalama vya Somalia huko Dhobley mnamo Jumatano vilimkamata mwanamke na wanaume wawili wanaotuhumiwa kufanya mipango ya kushambulia eneo hilo na jirani Kenya, Redio Bar-Kulan inayofadhiliwa na Umoja wa Mataifa iliripoti.
Washukiwa hao ilisemekana wako katika hatua za mwisho za kupanga mfululizo wa mashambulio, kwa mujibu wa ofisa wa serikali ya Dhobley, Hanad Farah. Farah alisema serikali hiyo itaendelea kuchukua hatua kali za kinidhamu dhidi ya wapiganaji wa al-Shabaab wanaoshukiwa na wafuasi wao.
Polisi nchini Tanzania wamewakamata watu 90 siku moja baada ya maandamano ambapo mtu mmoja aliuaw...
Kenya ililiomba Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa siku ya Alhamisi (tarehe 23 Mei) kufutwa kw...
Rais Hassan Sheikh Mohamud wa Somalia aliongoza sherehe za maadhimisho ya miaka 50 ya kuanzishwa ...
Mawaziri wa mambo ya nje wa mataifa wanachama wa Shirika la Maendeleo la Pembe ya Afrika (IGAD) w...
Kiongozi wa jamii huko Zanzibar, Mohammad Omar Said, alishambuliwa kwa tindikali siku ya Alhamisi...
Mahakama moja ya Puntland imewahukumu kifo watu saba kwa mauaji ya ulamaa wa Kisomali, Abdulkadir...
Shirika la kimataifa la misaada la Global Partnership for Education (GPE) limetangaza msaada wa d...
Shirika la kimataifa la kuteteta haki za binadamu la Amnesty International limetoa wito kwa Kenya...
Makamu wa Rais wa Kenya William Ruto ameahidi adhabu kali zaidi kwa majangili katika mswada wa Sh...
Raisi wa Kenya Uhuru Kenyatta siku ya Alhamisi (tarehe 23 Mei) alitoa majina mawili ya mwisho ya ...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji