Jeshi la Polisi Tanzania kuchunguza vyeti vya masomo vilivyoghushiwa

Mei 16, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Mpelelezi Mkuu wa Polisi nchini Tanzania (IGP) Saidi Mwema ameunda timu ya kuchunguza tuhuma za vyeti vilivyoghushiwa na baadhi ya maofisa wa Jeshi la Wananchi la Tanzania, gazeti la Daily News la Tanzania liliripoti siku ya Jumatano (tarehe 16 Mei).

"IGP ameunda timu ya kuchunguza kashfa hii ili kuhakikisha uvumi huo wa kugushi, timu hiyo imeanza kazi yake mara moja leo," msemaji wa polisi Advera Senso alisema siku ya Jumanne.

Kashfa hiyo ilitangazwa na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa, ambayo iligundua kwamba zaidi ya maofisa 700 wa polisi na takriban wanajeshi wa jeshi la ulinzi 250 walishushi vyeti vyao za masomo.

Senso alisema hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi ya wale wote waliokamatwa kughushi vyeti vyao vya masomo.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 2)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo

Nyenzo