Mei 16, 2012
Mpango wa Chakula Duniani (WFP) wameanza mradi mpya nchini Somaliland kuwapa maelfu ya watu vocha za kununua nyama mbichi na vyakula kutoka kwa wauzaji wa ndani, Umoja wa Mataifa ulitangaza siku ya Jumanne (tarehe 15 Mei).
"Kutumia vocha kunawapa watu uchaguzi wa chakula gani cha kukiwa na kutoa nyenzo mpya yenye nguvu kwa WFP kwa ajili ya kutoa msaada wa chakula kwa wale waliopo katika mazingira magumu zaidi," alisema Mkurugenzi wa WFP nchini Somalia Stefano Porretti. "Wakati huohuo, vocha zinasaidia uchumi wa nchi kwa kuwasaidia wazalishaji wadogo na wa kiwango cha kati na wachuuzi wa nchini."
Wasomali 15,000 waliosajiliwa katika programu hiyo watapokea Dola za Marekani 80 kwa vocha kila mwezi, ambazo wanaweza kutumia katika ununuzi wa mchele, mafuta ya kula na nyama. WFP ina mpango wa kupanua programu ambayo inasemekana kuwa imefanikiwa kuwa mbadala wa uwiano wa chakula.
WFP inashirikiana na Baraza la Wakimbizi la Denmaki kusambaza vocha hizo, kwa kushirikiana na Medair, asasi isiyo ya serikali ambayo inasimamia programu ya lishe huko Burao, ambako awamu ya kwanza ya programu ya vocha imeanza.
WFP imepanga kutumia programu ya vocha katika nchi nzima, ambako hali ya soko inaruhusu.
Baadhi ya wabunge wa Somalia wameitupilia mbali hoja ya kumtaka waziri mkuu na baraza lake la maw...
Wabunge wa upinzani walidai kwamba serikali ya Tanzania imekuwa ikibana uhuru wa kujieleza na kud...
Sampuli ya DNA iliyochukuliwa kwenye mswaki uliokuwemo kwenye begi lililokuwa na risasi lililopat...
Wakenya kumi na wasaba wameshtakiwa kwa kuvunja amani, kufanya ghasia na ukatili dhidi ya wanyama...
Al-Shabaab imedai kuhusika na urushwaji wa makombora kwenye kasri ya rais mjini Mogadishu siku ya...
Wanajeshi wa Uganda wa Kikosi Namba 9+ wanarudi nyumbani baada ya kukamilisha miezi 13 ya ziara y...
Kikosi cha polisi cha Kenya kitaanza uhakiki wa kina wa maofisa mwezi ujao, kikianza na kusaili w...
Ujambazi ulizuiwa katika ofisi za usalama za Wells Fargo huko Mombasa ulisababisha kifo cha watu ...
Rais wa Ghana John Dramani Mahama aliahidi msaada wa nchi yake katika kipindi cha ujenzi mpya wa ...
Polisi nchini Tanzania walimkamata mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msingwa, na wafanyabiashara 60 k...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji