Polisi wa Kenya wamkamata mshukiwa mmoja katika shambulio la bomu kwenye mgahawa huko Mombasa

Mei 16, 2012

  • 1 Maoni
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Polisi wa Kenya walimkamata mwanaume anayeshukiwa kuwa amehusika katika shambulio la bomu katika mgahawa huko Mombasa ambalo lilimuua mwanamke mmoja na kujeruhi watu watatu, Mkuu wa Polisi Mathew Iteere aliwambia waandishi wa habari Jumatano (tarehe 16 Mei).

Katika shambulio hilo la Jumanne jioni, mwanaume mwenye silaha alipiga risasi mgahawa wa Vista Belle, wakati walinzi wa usalama walipomzuia na washiriki wake wawili kutoingia katika mgahawa huo. Washiriki hao wawili katika jinai hiyo walirusha mabomu kwenye mgahawa huo na kukimbia.

Moja ya bomu lililipuka karibu na mlango wa kuingia kwenye mgahawa na lingine karibu na sehemu ya maegesho ya magari nje.

Tumempoteza mmoja wa waathirika, msichana ambaye alikuwa mlinzi wa klabu hii, alifia hospitalini,” mkuu wa polisi wa kanda Aggrey Adoli aliiambia AFP.

Majeruhi watatu wamebakia hospitali, mmoja ana hali mbaya. “Mshukiwa huyo ni mmoja wa wale waliojeruhiwa,” Iteere alisema. “Kwa sasa yuko chini ya ulinzi wa polisi."

Mshukiwa alikuwa amekata tiketi ya basi kuondoka Mombasa mara tu baada ya shambulio, Iteere alisema.

“Tumeipata tiketi ya basi na wakati maofisa wetu walipokwenda kituo cha basi, waliikuta mizigo yake, ambayo ilikuwa na bunduki iliyokuwa imejazwa mizunguko minane ya risasi," alisema. "Pia tulipata kompyuta ya mkononi kutoka kwake ambayo sasa tunaichunguza.”

Iteere alisema polisi wamekuwa wakimtafuta mshukiwa “kuhusiana na mashambulio mengine kadhaa”.

Hakuna kundi lililodai kuhusika, ingawaje Kituo cha Vijana wa Kiislamu cha Kenya, kundi linalohusishwa na al-Shabaab, wanaelekea kufanya shambulio hilo.

"Asubuhi hii, nani wanafurahi na nani wanaoomboleza? Fikiria kuhusu jambo hili. Tokeni Somalia!” ujumbe mmoja katika mtandao wa Twitter ulisomeka hivyo. Bomu moja au mawili katika eneo sahihi na sauti yake husikika kwenye uchumi wa Kenya.”

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Maoni ya msomaji

  • eddy
    May 17, 2012 @ 02:06:10PM

    Haya ni matendo ya uoga na matendo kama haya msiyavumilie.

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo

Nyenzo