Mei 15, 2012
Zaidi ya askari 600 wa Somalia walimaliza mafunzo ya kijeshi ya miezi sita nchini Uganda hapo tarehe 10 Mei na wanarejea nyumbani ili kukuza vikosi vya usalama vinavyopambana na al-Shabaab.
Kanali Winston Byaruhanga, mkuu wa shule ya mafunzo ya kijeshi ya Bihanga katika wilaya ya Ibanda, aliiambia idara ya habari ya IRIN kuwa mpaka mwisho wa mwaka, kiasi cha askari 3,000 na maafisa watapatiwa mafunzo ya kijeshi. Alisema kuwa askari 603 wa Somalia waliopatiwa mafunzo na askari 248 wa Uganda watasaidia kuleta amani na utulivu nchini Somalia.
“Askari hawa wanaunda sehemu muhimu ya jeshi la Somalia. Waambie al-Shabaab wako wapi, nao wako tayari kwa kazi,” alisema Luteni Jenerali Edward Katumba Wamala, kamanda wa Vikosi vya Miguu vya Uganda. “Askari hawa wataleta amani nchini Somalia. Sisi tuna msimamo hasi kuwa amani itapatikana Somalia karibuni.”
Mafunzo hayo ni pamoja na mazoezi ya vita vya mjini, kufahamu mabomu ya kuzikwa, afya, elimu ya siasa na silaha.
“Tumedhamiria kurejea nyumbani na kulinda amani nchini kwetu kutoka kwa al-Shabaab,” alisema askari wa Somalia Mohammed Ali Hassan, aliyetambuliwa kama mwanafunzi bora wakati wa mafunzo. “Sasa tumeshajengwa na tuko tayari kwa vita.”
Ujumbe kutoka Jumuiya ya Maendeleo ya Pembe ya Afrika (IGAD) uliwatembelea maafisa mjini Mogadish...
Mshukiwa wa ugaidi na mke wake walipigwa risasi na kufa na maafisa sita wa polisi walijeruhiwa wa...
Watu watano walikamatwa siku ya Jumanne mjini Dar es Salaam wakiwa na vifaa vya kulipua katika mi...
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta aliwataka wabunge kuweka kando madai yao ya kuongezwa mishahara kwa ...
Majeshi ya serikali ya Somalia waliwaua wanamgambo tisa wa al-Shabaab wakati wa mapambanao hapo J...
Mtu asiyejulikana alimpiga kwa risasi na kumuua ofisa wa kitengo cha usalama cha kijeshi huko kas...
Muungano wa Jubilee tawala cha Kenya kilichukua uongozi wa kamati mbili muhimu za bunge Ijumaa (t...
Chama cha Wafanyabiashara na Asasi ya Chakula na Kilimo ya Umoja wa Mataifa vinatoa mafunzo kwa w...
Balozi wa Umoja wa nchi za Ulaya nchini Tanzania Filiberto Ceriani Sebregondi aliwahamiza waandis...
Makamu wa Rais wa Kenya, William Ruto, alisema kazi za Misheni ya Umoja wa Afrika nchini Somalia ...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji