Umoja wa Mataifa, Serikali ya Somalia zasaini makubaliano ya haki za binadamu

Mei 13, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Mashirika kadhaa ya Umoja wa Mataifa yamesaini taarifa ya makubaliano na serikali ya Somalia siku ya Ijumaa (tarehe 11 Mei) kuomba uimarishaji wa haki za binadamu nchini, Redio Bar-Kulan inayodhibitiwa na Umoja wa Mataifa iliripoti.

Makubaliano hayo yalifikiwa kwa ombi la serikali ya Somalia, na yatarahisisha uimarishaji wa maeneo saba makuu, ikiwa ni pamoja na kuimarisha utawala wa sheria na usimamiaji wa haki, kuvilinda vikundi vinavyoweza kudhurika kirahisi – ikiwa ni pamoja na wanawake, watoto, watu wa ndani ya nchi waliokimbia makazi yao na waandishi wa habari – pamoja na utekelezaji wa mikataba ya kimataifa juu ya haki za binadamu.

“Msaada wa kiufundi utatolewa katika njia ambayo itahakikisha umuliki wa kitaifa, ushiriki, uwazi na ujumuishaji wa wadau muhimu, hasa kuhusiana na vipaumbele vilivyokubaliwa katika kila eneo,” makubaliano hayo yanasomeka.

Makubaliano hayo yalitiwa saini huko Mogadishu na Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu, Ofisi ya Kisiasa ya Umoja wa Matiafa Somalia na serikali ya Somalia.

Waziri Mkuu wa Somalia Abdiweli Mohamed Ali alielezea ahadi za serikali yake katika kuimarisha na kulinda haki za binadamu katika taarifa kwa waandishi wa habari baada ya kusaini makubaliano hayo.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo