Ungependa kuifanya Kiswahili kuwa lugha ya chaguo lako, katika tovuti hii? |
Mei 13, 2012
Meli ya jeshi la maji ya Uholanzi ya Van Amstel siku ya Ijumaa (tarehe 11 Mei) iliwaachia huru mabaharia 17 ambao walitekwa na watuhumiwa wa uharamia nje ya pwani ya Somalia, Waziri wa Ulinzi wa Uholanzi alisema.
"Mabaharia hao walioachiwa huru wanaendelea vizuri wakizingatia mazingira hayo na wanaendelea na safari," wizara ilisema, ikitangazwa na HAbari ya BNO News ya Uholanzi. "Watuhumiwa hao wa uharamia walihamishiwa katika manoari ndogo ya kusindikiza. Kwa sasa wafanyakazi wa misheni ya Umoja wa nchi za Ulaya Atalanta wanajadiliana uwezekano wa kuwashitaki watuhumiwa wa uharamia."
Wizara ilisema watuhumiwa 11 wa uharamia walichukuliwa katika uangalizi, na kukamata silaha za baharini, baruti na vitu vingine vinavyoweza kutumika katika uharamia.
Utaifa wa mabaharia hao na muda waliochukuliwa mateka havikupatikana mapema.
Raisi wa Kenya Uhuru Kenyatta siku ya Alhamisi (tarehe 23 Mei) alitoa majina mawili ya mwisho ya ...
Watu watano waliuawa na wanne kujeruhiwa katika mashambulizi mawili kwenye eneo la kaskazini mash...
Sababu kuu ya vurugu ambazo ziliua zaidi ya watu 150 katika Delta ya Mto Tana mwaka jana ilitokan...
Shirika la Afya Duniani (WHO) lilitangaza mlipuko wa polio katika Pembe ya Afrika siku ya Jumatan...
Majeshi ya serikali ya Somalia yamezifungia kampuni za mawasiliano ya simu na biashara nyingine h...
Serikali ya Somalia itaanza kuunda tawala za kikanda katika maeneo yaliyokombolewa kutoka kwa al-...
Waziri wa Nishati wa Djibouti Ali Yacoub Mohamoud na Balozi wa Japani nchini Djibouti Atsushi Nis...
Ufunguzi wa Mkutano wa Wasambazaji wa mafuta na gesi Tanzania utafanyika huko Dar es Salaam tareh...
Wabunge wameondoa hoja yao inayomtaka Waziri Mkuu Abdi Farah Shirdon na baraza lake la mawaziri k...
Rais Ahmed Silanyo wa mkoa wa Somaliland alikutana na Mwakilishi Maalum wa Umoja wa Ulaya kwa Som...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji