Mei 13, 2012
Usambazi maji mjini Nairobi utaendelea kuathiriwa na kukatika katika kwa wiki mbili zijazo baada ya mafuriko kuharibu bomba kubwa kutoka bwawa la Sasumua kuelekea sehemu za kusini na magharibi ya jiji hapo Jumanne, Redio Capital News FM ya Kenya iliripoti hapo Jumamosi (tarehe 12 Mei).
Mkurugenzi Mwendeshaji wa Kampuni ya Maji Safi na Maji Taka Philip Gichuki aliwaambia waandishi wa habari kuwa maeneo yaliyoathiriwa yatapata maji kwa masaa 36 kila wiki. Alitoa tahadhari kwa wakazi wa mjini watumie maji kwa uangalifu, ingawa alihakikisha kuwa bei ya maji itabakia ile ile.
"Hili ni suala la dharura na tutabeba gharama ambazo zitatokea ingawaje hatuwezi kusema kwa sasa zitakuwa kiasi gani," alisema.
Maeneo yaliyoathiriwa ni pamoja na Karen, Westlands, Gigiri, Chuo Kikuu cha Nairobi, Lavington, Kawangware, Upperhill, Hospitali ya Taifa ya Kenyatta, Dagoretti Corner, Ngong Road Idara ya Ulinzi.
Bwawa la Sasumua ni la pili kwa ukubwa nchini, linalosukuma lita milioni 60 kwa siku na kutoa sehemu mbili kati ya tatu katika hifadhi ya maji ya Kabete kuelekea magharibi ya Nairobi.
Makamu wa Rais wa Kenya, William Ruto, alisema kazi za Misheni ya Umoja wa Afrika nchini Somalia ...
Rais Hassan Sheikh Mohamud wa Somalia siku ya Alhamisi (tarehe 16 Mei) alipokea vyeti vya utambul...
Kwa uchache watu wanne waliuawa na watatu kujeruhiwa siku ya Alhamisi (tarehe 16 Mei) baada ya wa...
Kenya na Tanzania zilifanya operesheni ya pamoja ya ulinzi wa mpaka siku ya Alhamisi (tarehe 16 M...
Mwanachama wa kundi la wanamgambo wanaoiunga mkono serikali ya Somalia la Ahlu Sunna wal Jamaa, A...
Wanawake watatu waliuawa usiku wa Alhamisi (tarehe 16 Mei) katika eneo la Malkamau kwenye Kaunti ...
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon. siku ya Alhamisi (tarehe 16 Mei) alimteua waziri wa...
Tanzania na Canada zimesaini mkataba wa ushirikiano yanayokusudiwa kuimarisha na kuunda mazingira...
Jeshi la Taifa la Somalia liliwauwa wanamgambo 13 wa al-Shabaab siku ya Jumanne (tarehe 14 Mei), ...
Muda wa mwisho kwa wakaazi wa Mandera kusalimisha silaha zao haramu umeongezwa hadi Ijumaa (tareh...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji