Taarifa ya Kenya yaonyesha kuboreshwa kwa usimamizi wa kodi

Mei 08, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Taarifa ya utafiti uliotolewa na Chama cha Walipakodi cha Taifa Kenya siku ya Jumatatu (tarehe 7 Mei) uligundua kwamba kuimarishwa kwa uchunguzi wa umma na mashtaka ya watuhumiwa wa ubadhilifu wa mali ya umma umepunguza matumizi mabaya ya fedha.

Hata hivyo, taarifa hiyo ilionyesha kwamba shilingi milioni 363 (Dola za marekani milioni 4.3) zilitumika vibaya katika mwaka wa fedha wa 2009-2010, gazeti la Business Daily Africa liliripoti.

Chama hicho kilifanya utafiti wa majimbo 38 na kiligundua kwamba jimbo la uchaguzi la Gatanga lilikuwa la kwanza kwa matumizi mazuri ya Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo (CDF) na Mfuko wa Kuhamisha Mamlaka ya Ndani, bila kuwa na tukio la matumizi mabaya ya fedha.

Wundanyi, lilikuwa ni jimbo la pili ambalo mbunge wake alipongezwa kwa kuruhusu wapiga kura kuchagua wajumbe wa kamati ya CDF. "Kila kundi limewakilishwa, ndiyo maana tuna utendaji mzuri," mbunge wa Wundanyi Thomas Mwadeghu alinukuliwa akilieleza gazeti la Daily Nation la Kenya.

Marakwet Mashariki lilikuwa ni jimbo lililofanya vibaya kuliko yote kwa takriban asilimia 50 ya fedha za CDF hazikutumika vizuri.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo