Mkimbiaji wa Kenya aweka rikodi Berlin

Mei 07, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Mwanariadha wa Kenya, Dennis Kimetto, ameweka rikodi mpya ya dunia hapo Jumapili (tarehe 6 Mei) kwa mbio za kilomita 25 kwenye Uwanja wa Olimpiki wa Berlin, Ujerumani, akitumia saa 1, dakika 11 na sekunde 18.

Kimetto, mwenye umri wa miaka 28 aliivunja rikodi iliyowekwa na Mkenya mwenzake Sammy Kosgei miaka miwili iliyopita huko Berlin kwa kukimbia kwa saa 1, dakika 11 na sekunde 50.

Kimetto alikimbia sambamba na Wakenya wengine wawili, Wilfred Kigen na Jacob Kendagor, ambao walipata nafasi za pili na tatu. Kigen pia alivunja rikodi ya hapo kabla kwa kukimbia kwa saa 1 dakika 11 na sekunde 29.

“Ilikuwa lengo letu kuvunja rikodi,” alisema Kimetto, kwa mujibu wa Shirika la Kimataifa la Riadha. “Tulijua ndani ya mashindano yote kuwa tutaweza kufanya hivyo.”

Mkenya Caroline Chepkwony, mwenye umri wa miaka 27, alichukuwa nafasi ya kwanza katika mbio za wanawake akitumia saa 1, dakika 22 na sekunde 56.

“Hili ni jambo kubwa na lilikuwa la kasi sana. Nilikimbia kwa dakika moja mbele zaidi kuliko nilivyopanga,” alisema Chepkwony.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 1)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo

Nyenzo