Mei 07, 2012
Polisi wa Kenya wamemtambua mshukiwa katika shambulio la kombora la tarehe 29 Aprili katika kanisa huko Nairobi kuwa ni wakala wa al-Shabaab.
Mshambuliaji, ambaye kwa jina la lakabu anajiita “Amar” alikuwa Kismayo, Somalia mwaka uliopita lakini alirudi Kenya mapema mwaka huu, Kamishina wa Polisi Matthew Iteere alisema.
Polisi wametoa picha ya mshukiwa huyo na kutoa wito kwa mtu yeyote mwenye ufahamu ambao utasaidia kukamata kwake kuwezekana, “Ni muhimu kuzingatia kuwa ni mtu hatari na anayeaminika kuwa na silaha aina ya bastola na inawezekana kuwa na mlipuko,” Redio Capital FM ya Kenya ilimnukuu Iteere akisema.
Shambulio hilo Kanisa la Kimataifa la Nyumba ya Miujiza ya Mungu katika eneo la Ngara lilimuua mtu mmoja papo hapo na kujeruhi 15.
Iteere alisema kiongozi wa al-Shabaab huko Kismayo “alidai kuhusika na shambulio hilo na akaapa kufanya mashambulio zaidi ya mabomu ya kujitoa muhanga kwa Kenya”.
Nairobi imeshuhudia mashambulio kadhaa ya mabomu katika maeneo ya raia tangu mwisho wa mwaka 2011, ambapo mlipuko ulioua watu tisa katika kituo cha basi mwezi Machi.
Raisi wa Kenya Uhuru Kenyatta siku ya Alhamisi (tarehe 23 Mei) alitoa majina mawili ya mwisho ya ...
Watu watano waliuawa na wanne kujeruhiwa katika mashambulizi mawili kwenye eneo la kaskazini mash...
Sababu kuu ya vurugu ambazo ziliua zaidi ya watu 150 katika Delta ya Mto Tana mwaka jana ilitokan...
Shirika la Afya Duniani (WHO) lilitangaza mlipuko wa polio katika Pembe ya Afrika siku ya Jumatan...
Majeshi ya serikali ya Somalia yamezifungia kampuni za mawasiliano ya simu na biashara nyingine h...
Serikali ya Somalia itaanza kuunda tawala za kikanda katika maeneo yaliyokombolewa kutoka kwa al-...
Waziri wa Nishati wa Djibouti Ali Yacoub Mohamoud na Balozi wa Japani nchini Djibouti Atsushi Nis...
Ufunguzi wa Mkutano wa Wasambazaji wa mafuta na gesi Tanzania utafanyika huko Dar es Salaam tareh...
Wabunge wameondoa hoja yao inayomtaka Waziri Mkuu Abdi Farah Shirdon na baraza lake la mawaziri k...
Rais Ahmed Silanyo wa mkoa wa Somaliland alikutana na Mwakilishi Maalum wa Umoja wa Ulaya kwa Som...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji
Maoni ya msomaji
Wakenya wengi wasio na hatia wameteseka kutokana na mashambulizi ya al-Shabaab, kwa hivyo wahalifu kama hao lazima wakamatwe na kushughulikiwa ipasavyo, na wale watakaoonekana na makosa wahukumiwe kifo.
Ajira za serikali zinawezekana kwa kupunguza ajira zinazosababisha vijana kujiunga na kikundi cha kigaidi ili waweze kuishi na kujikimu.