Mogadishu yarejea katika hali ya kawaida baada ya kuondolewa kwa al-Shabaab

Mei 06, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Mogadishu inarejea katika maisha ya kawaida wakati ujenzi mpya unaendelea na bei za mali zisizohamishika kupanda, AFP iliripoti hapo Jumamosi (tarehe 5 Mei).

“Watu wanajenga upya nyumba zao,” alisema msemaji wa serikali Abdurahman Omar Osman. “Wasomali waliokuweko uhamishoni wanarejea…biashara zinafunguliwa upya,” alisema.

“Siku hizi hakuna ukosefu wa ajira, ujenzi umeshamiri, “ fundi rangi Adan Sharif aliiambia AFP, na kusema kuwa sasa ana uhakika wa kuajiriwa kwa kazi mpya.

“Majengo mengi katika mtaa wetu yamekarabatiwa katika wiki za karibuni na yamekaa vizuri; eneo hilo haliko tena kama lilivyokuwa baada ya vita,” alisema Fadumo Moalim, mama wa watoto nane anayeishi katika wilaya ya Wardhigley.

Askari wa AMISOM na TFG waliwatimua al-Shabaab kutoka ngome zao za mwisho zilizobakia mjini Mogadishu mwezi Machi.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo