Kenya ilidhibiti sera za fedha mwezi Aprili

Mei 04, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Benki Kuu ya Kenya inaendelea na kiwango cha ukopeshaji cha asilimia 18 ili kudhibiti mfumko wa bei, Gavana wa Benki Kuu Njuguna Ndung’u alitangaza.

Ndung'u, anayeongoza Tume ya Sera ya Fedha (MPC), alisema upanuzi wa mikopo haujapungua na lengo la mfumko wa bei kwa asilimia 9 halijafikiwa ili kuthibitisha mwanzo wa kupunguza mzunguko, gazeti la Business Daily Afrika liliripoti hapo Alhamisi (tarehe 3 Mei). Kiwango cha mfumko wa bei kiko juu ya lengo, kwa asilimia 9.94.

Kiwango cha upanuzi wa mkopo kilibakia kuwa asilimia 24 mwezi Machi, juu ya lengo lililowekwa la asilimia 22, kwa mujibu wa takwimu rasmi. MPC imesema inapanga kupunguza kiwango cha mkopo kwa asilimia 18 ifikapo mwezi Juni.

“Tume iligundua kuwa kuna haja ya kuendelea na msimamo wa sera ya fedha ya sasa ili kuhakikisha kuwa mfumko wa bei unaendelea kushuka kufikia lengo na kuendeleza utulivu katika kiwango cha ubadilishaji fedha,” Ndung’u alisema.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo