Mafuriko makubwa Kenya na maporomoko ya ardhi vyawakosesha makazi watu 60,000

Mei 04, 2012

  • 1 Maoni
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Zaidi ya watu 40 wamekufa na 60,000 kukosa makazi baada ya mafuriko makubwa na maporomoko ya ardhi kuzikumba sehemu kadhaa za Kenya, gazeti la Daily Nation la Kenya liliripoti Alhamisi (tarehe 3 Mei).

Watu wawili wameripotiwa kupotea na 42 wamejeruhiwa, alisema msemaji wa Chama cha Msalaba Mwekundu Kenya Nelly Muluka. Alisema nyumba za takribani familia 100 pia zilisombwa na maji ya mafuriko.

"Kufuatia ukosaji wa makazi, chama kimekuwa kikigawa pamoja na vitu vingine, maturubai, mablanketi, vyandarua, vyombo vya jikoni na madumu yanayokunjika kwa familia zilizoathirika,” Mulika alisema.

Kina cha maji katika Mto Nzoia kimeongezeka kwa kiasi cha mita tano, “ambayo ni hali inayotisha,” alisema.

"Kufuatia kuongezeka kwa kina cha maji, watumishi wa Msalaba Mwekundu wamezishauri jamii ambazo ziko katika hatari kwenda sehemu za miinuko,” Muluka alisema.

Siku ya Alhamisi Shirika la Msalaba Mwekundu walizindua kituo cha afya kwa wakazi wa Nyanza ambao waliharibiwa makazi yao na mafuriko.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 1)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Maoni ya msomaji

  • JULIUS M
    May 7, 2012 @ 05:34:18AM

    MWISHO WA MTUME WA BWANA, DK. DAVID EDWARD OWOUR, ALIBASHIRI MAFURIKO YA KUTISHA KUJA ULIMWENGUNI KUTOKANA NA DHAMBI YA NGONO KATIKA ARDHI MIONGONI MWA MADHAMBI MENGINE. SASA HILI LIMETIMIA, WATU WOTE WANAPASWA KUFAHAMU KUWA KUNA MTUMISHI WA KWELI WA MUNGU HAPA DUNIANI, NA KILA MTU ANAPASWA KUITIKIA WITO WAKE KWA KUTUBU NA KUTAYARISHA NJIA KWA AJILI YA MESIA ANAYEKUJA.

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo