Mei 04, 2012
Wawakilishi kutoka vyombo vya habari vya Somalia, Chama cha Taifa cha Waandishi wa Habari Wasomali na Wizara ya Habari walitoa taarifa rasmi ya pamoja Alhamisi (tarehe 3 Mei) kuadhimisha Siku ya Vyombo vya Habari Duniani, ambapo walikubaliana kuendeleza uhuru wa vyombo vya habari.
Kufuatia mkutano kati ya waandishi wa habari na wawakilishi wa wizara, pande mbili ziliamua kwamba “vyombo vya habari vina nafasi kubwa katika kuimarisha amani na kuhimiza kuheshimu utawala wa sheria, hasa katika kipindi hiki kigumu cha utawala wa mpito.”
Chama pia kiliitaka serikali kutoa ulinzi zaidi kwa waandishi wa habari. Wanahabari watano wameuawa nchini Somalia mwaka huu, na mauaji ya hivi karibuni ni Jumatano huko Galkayo.
Mwakilishi Maalumu wa Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika nchini Somalia Balozi Boubacar Gaoussou Diarra aliwapongeza waandishi wa habari wa Somalia kwa nafasi yao muhimu katika kutangaza amani. “Inatia moyo kujua kiwango kikubwa cha bidii na shauku inayoonyeshwa na waandishi wa habari nchini Somalia licha ya mazingira ya hatari wanayofanyia kazi,” alisema katika taarifa yake.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon alionyesha kuchukizwa na kuongezeka kwa idadi ya waandishi wa habari wanaouawa wakati wakifanya kazi yao.
"Kinga ya kutoshitakiwa kwa wale wanaowashambulia au kuwatishia waandishi wa habari linabakia kuwa tatizo linaloongezeka; ikiwa ni pamoja na mashambulizi yanayofanywa mchana, yakitoa ujumbe wa kikatili sana,” Ban alisema katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa huko New York.
Wabunge wameondoa hoja yao inayomtaka Waziri Mkuu Abdi Farah Shirdon na baraza lake la mawaziri k...
Rais Ahmed Silanyo wa mkoa wa Somaliland alikutana na Mwakilishi Maalum wa Umoja wa Ulaya kwa Som...
Ukiritimba na ukosefu wa ufanisi katika bandari ya Dar es Salaam unaigharimu Tanzania na nchi jir...
Viongozi wa mkoa wa Puntland walikutana siku ya Jumanne (tarehe 21 Mei) kuwashajiisha wanawake ku...
Wanajeshi wa Somalia na wa Misheni ya Umoja wa Afrika nchini Somalia (AMISOM) waliwakamata zaidi ...
Rais Ismail Omar Guelleh wa Djibouti alijadiliana ushirikiano wa kimkakati na Kanali Saleh Ben Na...
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta, vikosi vya usalama na mahakama vinapaswa kuomba radhi hadharani kut...
Waziri Mkuu wa Djibouti Abdoulkader Kamil Mohamed alitoa wito wa kuongezwa kwa ushirikiano katika...
Baadhi ya wabunge wa Somalia wameitupilia mbali hoja ya kumtaka waziri mkuu na baraza lake la maw...
Wabunge wa upinzani walidai kwamba serikali ya Tanzania imekuwa ikibana uhuru wa kujieleza na kud...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji