Mei 03, 2012
Shirika la Watoto la Umoja wa Mataifa (UNICEF) limeonya kwamba limepokea asilimia 12 tu kati ya lengo lake lililojiwekea la dola milioni 298 kwa ajili ya kazi za misaada ya kibinaadamu nchini Somalia mwaka huu, ambako kunawaweka maelfu ya watoto wa Kisomali katika hatari ya kufa njaa.
“Kazi hii inaendelea na ni operesheni kubwa sana inayoyaokoa maisha ya watoto kila siku,” alisema msemaji wa UNICEF Marixie Mercado. “Ikiwa hatukupata fedha, programu zetu zote zitapaswa kukatwa,” alisema. “Wale waliokosa chakula kwa kiwango kikubwa ndio walio wenye hatari ya kifo.”
Mercado alisema kiasi cha watoto 325,000 waliokosa chakula cha kutosha wako kwenye uhitaji mkubwa wa msaada.
Alisema ukosefu wa usalama umekuwa kikwazo katika kuwasaidia watoto wenye mahitaji. “Tuna watoto milioni 1.9 ambao hawajafikiwa na chanjo katika maeneo ya kusini na kati kwa sababu ya vikwazo vya kiusalama,” alisema.
Makamu wa Rais wa Kenya, William Ruto, alisema kazi za Misheni ya Umoja wa Afrika nchini Somalia ...
Rais Hassan Sheikh Mohamud wa Somalia siku ya Alhamisi (tarehe 16 Mei) alipokea vyeti vya utambul...
Kwa uchache watu wanne waliuawa na watatu kujeruhiwa siku ya Alhamisi (tarehe 16 Mei) baada ya wa...
Kenya na Tanzania zilifanya operesheni ya pamoja ya ulinzi wa mpaka siku ya Alhamisi (tarehe 16 M...
Mwanachama wa kundi la wanamgambo wanaoiunga mkono serikali ya Somalia la Ahlu Sunna wal Jamaa, A...
Wanawake watatu waliuawa usiku wa Alhamisi (tarehe 16 Mei) katika eneo la Malkamau kwenye Kaunti ...
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon. siku ya Alhamisi (tarehe 16 Mei) alimteua waziri wa...
Tanzania na Canada zimesaini mkataba wa ushirikiano yanayokusudiwa kuimarisha na kuunda mazingira...
Jeshi la Taifa la Somalia liliwauwa wanamgambo 13 wa al-Shabaab siku ya Jumanne (tarehe 14 Mei), ...
Muda wa mwisho kwa wakaazi wa Mandera kusalimisha silaha zao haramu umeongezwa hadi Ijumaa (tareh...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji
Maoni ya msomaji
Maelezo mazuri, yanajieleza yenyewe.
Al-Shabaab ni kikundi cha kifisadi na kinachotesa watu. Hawawezei daima kujihesabu kuwa ni mujahidina na inatosha kuona wanayakataza mashirika ya misaada ya Kiislamu yaliyokuwa yanaingia eneo lao. Wanataka watu wafe kwa njaa, jambo linalothibitisha kuwa hawana ubinadamu wala hawana hisia, au fikra. Hatusemi lolote bali tunategemea msaada wa Mungu kutusaidia dhidi yao, kwa sababu wamezichafua akili za vijana na kuwafanya waharibu nyumba yao kwa mikono yao wenyewe.