Luteni Jenerali wa Uganda achukua uongozi wa AMISOM

Mei 03, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Luteni Jenerali wa Uganda Andrew Gutti alichukua uongozi wa jeshi la AMISOM siku ya Jumatano (tarehe 2 Mei) wakati wa sherehe za makabidhiano nchini Mogadishu, Umoja wa Afrika ulitangaza katika ujumbe wake.

"Lutenu Jenerali Gutti ataongoza majeshi ya AMISOM katika mapigano yanayoendelea ya kuleta amani na mafanikio kwa watu wa Somalia," balozi wa Umoja wa Afrika (AU) Rodney Kiwa aliwaambia viongozi wa Afrika na Umoja wa Matafia waliohudhuria.

"Pamoja na msaada wa jumuiya ya kimataifa, AMISOM wataendelea kufanya kazi ya kuleta amani na uhuru kwa Somalia kwa ajili ya siku zijazo, ambayo ni muhimu kwa maendeleo katika mapambano ya dunia dhidi ya ugaidi na kutafuta uimara wa kanda," alisema.

Gutti alifanya kazi kwa zaidia ya miaka 26 katika jeshi la Uganda na ataongoza jeshi lililopanuliwa la AMISOM lenye wanajeshi kutoka Kenya, Uganda, Jibuti, Burundi and Sierra Leone. Amepokea kutoka kwa Meja Jenerali Fred Mugisha, ambaye alisimamia ufukuzwaji wa wanamgambo wa al-Shabaab huko Mogadishu.

Jeshi la AMISOM kwa sasa lina wanajeshi 14,400 katika nchi kavu ya Somalia, lakini linaongezeka hadi takriban wanajeshi 18,000.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 4)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo