Waathirika wa bomu la Dhusamareb wapelekwa kwa ndege Nairobi, Addis Ababa

Mei 03, 2012

  • 1 Maoni
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Waathirika kadhaa wa bomu la kujitoa muhanga la Dhusamareb siku ya Jumanne walipelekwa kwa ndege Ethiopia kwa matibabu, na wengine walipangwa kupelekwa Nairobi, Redio Bar-Kulan inayofadhiliwa na Umoja wa Mataifa iliripoti Jumatano (tarehe 2 Mei).

Waathirika walielezwa kuwa na hali mbaya sana baada ya ulipuaji wa bomu la kujitoa muhanga kwenye mgahawa mahali ambapo watunga sheria wenyeji walikutana na raia. Ndege ya kukodi iliwachukua majeruhi kutoka Guri El kuwapeleka kwenda Addis Ababa, Alisema Mkuu wa Wilaya Osman Isse Noor.

Waziri wa Habari wa zamani Ahmed Abdisalan na wabunge Hussein Samatar na Abdirizak Isaac Biihi ni miongoni mwa majeruhi wanaotibiwa huko Ethiopia.

Waathirika wengine watano watapelekwa kwa ndege Nairobi kwa matibabu.

Al-Shabaab walidai kuhusika na shambulio hilo, ambalo liliua watu wanane.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Maoni ya msomaji

  • Abdiqadir
    May 4, 2012 @ 09:16:38AM

    Hii ingepaswa kuwa funzo kwa wafuasi wa taaghuut.

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo