Ungependa kuifanya Kiswahili kuwa lugha ya chaguo lako, katika tovuti hii? |
Aprili 30, 2012
Polisi nchini Kenya wanamtafuta mtuhumiwa wa kwanza katika shambulio la guruneti katika kanisa la Nairobi siku ya Jumapili (tarehe 29 Aprili), wakilenga juu ya maelezo ya mashuhuda kuwa mtu mwenye umri wa miaka 20 hivi aliondoka kanisani muda mfupi kabla ya mlipuko.
"Polisi wanafuata maelezo muhimu yaliyotolewa na mashuhuda ili kumtambua mshambuliaji,” alisema msemaji wa polisi Eric Kiraithe, kwa mujibu wa gazeti la Kenya la Daily Nation.
Shambulio liliua mtu mmoja katika eneo hilo, na kujeruhi watu 15. Waathiriwa kumi na mbili walipelekwa katika Hospitali ya Taifa ya Kenyatta, ambapo mmoja alikufa kutokana na majeraha wakati wa shambulio, alisema S.M. Monda, daktari mpasuaji katika hospitali hiyo.
“Hili ni tendo la kigaidi,” alisema Makamo wa Raisi Kalonzo Musyoka, aliyekuwa miongoni mwa maafisa wa serikali waliowatembelea waathirika hospitalini. “Inasikitisha kuwa wamefikia hadi ya kushambulia watu hata wakiwa katika ibada. Hata hivyo, tunawaomba watu watulie nchini kote.”
Ujumbe kutoka Jumuiya ya Maendeleo ya Pembe ya Afrika (IGAD) uliwatembelea maafisa mjini Mogadish...
Mshukiwa wa ugaidi na mke wake walipigwa risasi na kufa na maafisa sita wa polisi walijeruhiwa wa...
Watu watano walikamatwa siku ya Jumanne mjini Dar es Salaam wakiwa na vifaa vya kulipua katika mi...
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta aliwataka wabunge kuweka kando madai yao ya kuongezwa mishahara kwa ...
Majeshi ya serikali ya Somalia waliwaua wanamgambo tisa wa al-Shabaab wakati wa mapambanao hapo J...
Mtu asiyejulikana alimpiga kwa risasi na kumuua ofisa wa kitengo cha usalama cha kijeshi huko kas...
Muungano wa Jubilee tawala cha Kenya kilichukua uongozi wa kamati mbili muhimu za bunge Ijumaa (t...
Chama cha Wafanyabiashara na Asasi ya Chakula na Kilimo ya Umoja wa Mataifa vinatoa mafunzo kwa w...
Balozi wa Umoja wa nchi za Ulaya nchini Tanzania Filiberto Ceriani Sebregondi aliwahamiza waandis...
Makamu wa Rais wa Kenya, William Ruto, alisema kazi za Misheni ya Umoja wa Afrika nchini Somalia ...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji
Maoni ya msomaji
Hili limepitiliza mno lakini Mwenyezi Mungu bado yuko hai na anaona hata pale macho ya binadamu hayawezi kuona, kwa hivyo watenda maovu lazima waelewe kuwa siku yao inakuja wakati ukweli utakapojitokeza wenyewe kama ambavyo chochote kilichomo katika giza kitakuja kwenye mwanga na kila mtu atalishuhudia hilo.
Al-Shabaab wameandikiwa kushindwa. Mungu anaziona njia zenu za uovu na hamtafika mbali zaidi.