Aprili 27, 2012
Vimelea vya malaria vinavyoua watu wengi Afrika vimeonyesha kukinzana na madawa mengi yenye nguvu yaliyoko sokoni, watafiti huko London walieleza hapo Ijumaa (tarehe 27 Aprili).
Wanasayansi wamegundua ukinzani huo katika dawa dhidi ya malaria katika uchunguzi wa damu kutoka wagonjwa 11 kati ya 28 ambao waliugua baada ya kutembelea nchi za Afrika chini ya jangwa la Sahara, hayo ni kwa mujibu wa machapisho katika Jarida la Malaria la BioMed Central.
"Ukinzani huo katika majaribio ya maabara kwa kawaida hupelekea kuwepo kwa ukinzani pia katika baadhi ya nyakati kwa mgonjwa," alisema mkuu wa utafiti huo Sanjeev Krishna, kwa mujibu wa AFP. "Hilo linaweza kumaanisha kushindwa katika matibabu, bado tuna haja ya kutathmini zaidi."
Ukinzani huo wa madawa kwa matibabu kumeibua wasiwasi kuhusu madawa kutokuwa na nguvu kwa wagonjwa, hasa katika nchi za Afrika chini ya Jangwa la Sahara, ambako aslimia 50 ya vifo vinavyotokana na malaria hutokea kila mwaka.
Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani, kulikuwa na vifo 655,000 vya malaria mwaka 2010. Malaria ni ya tano kwa kusababsha vifo vya kawaida katika nchi zinazoendelea.
Makamu wa Rais wa Kenya, William Ruto, alisema kazi za Misheni ya Umoja wa Afrika nchini Somalia ...
Rais Hassan Sheikh Mohamud wa Somalia siku ya Alhamisi (tarehe 16 Mei) alipokea vyeti vya utambul...
Kwa uchache watu wanne waliuawa na watatu kujeruhiwa siku ya Alhamisi (tarehe 16 Mei) baada ya wa...
Kenya na Tanzania zilifanya operesheni ya pamoja ya ulinzi wa mpaka siku ya Alhamisi (tarehe 16 M...
Mwanachama wa kundi la wanamgambo wanaoiunga mkono serikali ya Somalia la Ahlu Sunna wal Jamaa, A...
Wanawake watatu waliuawa usiku wa Alhamisi (tarehe 16 Mei) katika eneo la Malkamau kwenye Kaunti ...
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon. siku ya Alhamisi (tarehe 16 Mei) alimteua waziri wa...
Tanzania na Canada zimesaini mkataba wa ushirikiano yanayokusudiwa kuimarisha na kuunda mazingira...
Jeshi la Taifa la Somalia liliwauwa wanamgambo 13 wa al-Shabaab siku ya Jumanne (tarehe 14 Mei), ...
Muda wa mwisho kwa wakaazi wa Mandera kusalimisha silaha zao haramu umeongezwa hadi Ijumaa (tareh...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji