Tanzania yazindua kampeni ya chanjo bila malipo

Aprili 26, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Wizara ya Afya ya Tanzania inawahamasisha raia kushiriki katika programu ya wiki ya chanjo ambayo ilianza Jumatano (tarehe 25 Aprili).

Tunahitaji kuwapa chanjo watoto wote, ingawa tunawalenga akina mama ambao walikosa nafasi ya kuwapatie chanjo watoto wao chini ya programu za kawaida za chanjo,” Yussuf Makame wa Idara ya Programu Kubwa ya Chanjo alisema katika mkutano na waandishi wa habari siku ya Jumanne.

Uchanjaji bure umegongana na Wiki ya Chanjo Afrika, tarehe 23 – 29 Aprili. Huko Zanzibar, wizara inapewa chanjo kwa watoto wachanga wenye umri wa chini ya mwaka mmoja dhidi ya kupata magonjwa mbalimbali yakiwemo ya pepopunda, kifua kikuu, donda koo na surua. Makame alisema chanjo ni sehemu ya mpango wa nchi wa kufikia Malengo ya Maendeleo ya Milenia ya kupunguza vifo vya watoto kwa theluthi mbili ifikapo 2015.

Mapema wiki hii, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Hadji Mponda alisema programu za chanjo za Tanzania tayari zimeshapunguza kiwango cha vifo kwa watoto chini ya miaka mitano kwa zaidi ya asilimia 80 kutoka mwaka 1999 hadi 2000, gazeti la The Citizen la Tanzania liliripoti.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo

Nyenzo