Wapiganaji 3 wa al-Shabaab wakimbilia kwa vikosi vya Somalia

Aprili 26, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Wapiganaji watatu wa al-Shabaab huko ukanda wa chini wa Juba wamebadilisha uelekeo na kupokelewa na maofisa wa serikali ya mtaa, Redio Bar-Kulan inayofadhiliwa na Umoja wa Mataifa iliripoti Alhamisi (tarehe 26 Aprili).

Wapiganaji hao watatu waliojisalimisha huko Qoqani, awali waliripotiwa kwa Hassan Yukub, kamanda mwandamizi wa al-Shabaab . Wawili walikuwa wakifanyakazi katika kikosi chake cha usalama wakati yule watatu alikuwa dereva, Mohamed Addullah, ofisa wa jeshi wa Serikali ya Mpito ya Shirikisho aliimbia Bar-Kulan.

Wanaume hao walipokelewa vizuri na sasa wanashikiliwa katika kituo cha polisi cha mji huo, alisema.

Kuasi kwa wapiganaji hao kumekuja wiki moja baada ya viongozi wengine wawili wa al-Shabaab kujisalimisha kwa maofisa wa serikali huko Qoqani. Redio Bar-Kulan iliripoti. Serikali inadhania kuwa kuasi kwa hivi karibuni ni kwa sababu ya ahadi ya msamaha inayoendelea kwa mwanachama yeyote wa al-Shabaab anayeasi.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 2)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, serikali za majimbo ya shirikisho ziundwe vipi nchini Somalia kufuatia utata wa Jubbaland?

Angalia matokeo