Mamlaka ya Maendeleo ya Chai Kenya kuzalisha umeme wa nguvu za maji

Aprili 25, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Mamlaka ya Maendeleo ya Chai ya Kenya imepanga kujenga mtambo wa kuzalishia umeme wa nguvu za maji wenye thamani ya shilingi milioni 400 (Dola za Marekani milioni 4.8) kwa ajili ya viwanda vitatu huko Embu, mjumbe wa bodi Samuel Murithi Ireri alitangaza siku ya Jumanne (tarehe 24 Aprili).

Kutumia umeme wa maji utakaozalishwa kutoka katika Mto Thuci kutaokoa viwanda kwa zaidi ya shilingi milioni 54 (Dola za Marekeni 65,000) za bili za umeme kwa mwaka, pamoja na kuongeza mapato kwa kuuza umeme katika gridi ya taifa, Ireri alisema wakati wa uzinduzi wa wiki ya upandaji miti katika Mlima Kenya.

Itapunguza matumizi ya kuni na kupunguza mahitaji ya ukataji miti katika misitu ya Kenya," alisema. Wakulima wa eneo hilo hawataki kutegemea wakulima kupata kuni. Tunataka kuhakikisha msitu uliopo umebakiswa au kuongezekwa," alisema. Wakulima wa eneo hilo wanakusudia kupanda zaidi ya miti 450,000 msimu huu ili kufidia upungufu uliotokana na uchomaji wa mapori, alisema.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo