Halmashauri ya Mji wa Nairobi yapokea cheti cha kimataifa cha uthibitisho wa viwango

Aprili 25, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Halmashauri ya Mji wa Nairobi ilizawadiwa cheti cha Shirika la Kimataifa cha Uthibitisho wa Viwango (ISO) kwa utoaji wa huduma Jumanne (tarehe 24 Aprili), kufuatia jitihada zake za kurekebisha huduma za serikali na kuanzisha malipo kupitia katika njia za elektroni.

"Baraza la Mji wa Nairobi imekuwa kituo cha kwanza cha mji katika Afrika Mashariki na Kati kupata uthibitisho wa ISO,” Karani wa Mji Philip Kisia alisema alipopokea tuzo huko Ukumbi wa Jiji. “Hata hivyo, ushindi huu mkubwa na heshima vinakuja kwa wakati – kila baada ya miezi sita mchakato utakuwa ukipitiwa upya ili kuhakikisha ufuataji, hivyo hakuna nafasi ya kulala.”

Kisia alisema timu yake imeleta mabadiliko katika sekta muhimu tano ikiwa ni pamoja na fedha, teknolojia ya habari na mawasiliano, mipango, uthamini wa mali na rasilimali watu. Pia alitaja mafanikio yake katika kusambaratisha vikundi vya ufisadi.

Kisia alisema mapato ya halmashauri yataongezeka kwa shilingi bilioni 5 (kiasi cha Dola milioni 60) mara mfumo wa malipo kupitia elektroniki utakapozinduliwa wiki chache zijazo, gazeti la Daily Nation la Kenya liliripoti.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo