Qatar yasaidia dola za kimarekani 9000 kwa waandishi wa habari wa Somalia waliojeruhiwa.

Aprili 24, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Kituo cha Doha cha Uhuru wa Vyombo vya Habari kilitoa dola 9000 kwa msaada wa matibabu kwa waandishi wa habari sita waliojeruhiwa hapo tarehe 4 Aprili kwa bomu la kujitoa muhanga katika Jengo la Maonyesho la Taifa la Mogadishu, Redio RBC ya Somalia iliripoti hapo Jumatatu (tarehe 23 Aprili).

Chama cha Taifa cha Waandishi wa Habari wa Somalia (NUSOJ) iligawanya pesa hizo Ijumaa iliyopita kwa Said Warsame (Shuuriyaako), Deeqo Mohamed Ahmed, Ahmed Ali Kahiye, Hamdi Muhumad Hassan, Ayaan Abdulle Guure na Makamo wa Raisi wa NUSOJ Saleiban Sheik Ismail.

Warsame, aliyeungua vibaya mwili mwake, alipewa dola 2000 ili zimsaidie kutibiwa nje ya Somalia.

Katibu Mkuu wa NUSOJ Mohamed Ibrahim alikabidhi pesa hizo kwa mkurugenzi wa Royal International Television Abdulkadir Dulyar, ambaye aliziwasilisha katika familia ya Warsame.

"Kama unavyooana… wenzetu hawawezi kutibiwa Somalia na kwa niaba ya vyombo vya habari, ninayaomba mashirika yote na asasi za serikali zilizoguswa na suala hili kuwasaidia waandishi wa habari wa Somalia waliojeruhiwa,” Dulyar alisema.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo

Nyenzo