Viongozi wa Somalia wasifia vikosi vya jeshi kwenye kumbukumbu ya miaka 52

Aprili 23, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Rais wa Somalia Sheikh Sharif Sheikh Ahmed na Waziri Mkuu Abdiwei Mohamed Ali walitoa sifa kwa Vikosi vya Jeshi la Somalia, ambavyo viliadhimisha kumbukumbu yake ya Miaka 52 Jumatatu (tarehe 23 Aprili), Redio Bar-Kulan inayofadhiliwa na Umoja wa Mataifa iliripoti.

Watu hao wawili walizungumza wakati wa sherehe katika ufukwe wa Lido wa Mogadishu, ambayo ilijumuisha gwaride kwa vikosi vya Serikali ya Mpito ya Shirikisho.

Ahmed alisisitiza jukumu la vikosi hivi lililofanywa katika kuilinda Somalia na kukomboa Mogadishu kutoka kwa al-Shabaab. Rais pia alisifia jukumu la la AMISOM katika kutoa mafunzo kwa jeshi la Somalia kufuatia miongo miwili ya mgogoro.

Naye Waziri Mkuu Abdiwei Mohamed Ali alielezea furaha yake kwa kushuhudia kumbukumbu hii, akitoa wito kwa vikosi hivi kuendeleza kazi yake nzuri, ambayo alisema inasaida kurejesha utu wa Somalia.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 1)

Dislike_icon(1)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo