Kampuni ya Ufaransa yajenga bwawa huko Arusha

Aprili 22, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Bwawa linaloendelea na ujenzi katika mkoa wa Arusha Tanzania linatarajiwa kusambaza maji safi kwa watu wanaokadiriwa 5,000 kwa wakazi wa eneo hilo na ng'ombe 20,000, gazeti la Tanzania la The Guardian liliripoti hapo Jumamosi (tarehe 21 Aprili).

Kampuni ya Ufaransa ya Sogea-Satom, ambayo inakarabati barabara kuu ya Arusha-Minjigu, linajenga bwawa lenye thamani ya shilingi milioni 100 (sawa na dola za Kimarekani 63). Afisa uhusiano wa kampuni hiyo, Jamal Nassor Addi alisema bwawa hilo litamalizika katika muda wa wiki mbili, na unatarajiwa kudumu kwa miaka 120.

Bwawa hilo liko katika kijiji cha Nanja. "Eneo hili ni zuri kwa mifugo na mara tu maji yatakapokuwa tayari, tutakuwa na uwezo wa kujiletea maendeleo," alisema mweneyekiti wa kijiji hicho Ting'ine Shamburi.

Msemaji mwanamke wa kijiji cha Nanja, Bi. Rehema Sangar' alisema, "Nimefurahi sana kwa sababu adha yetu ya kuamka alfajiri sana na kutembea umbali wa kilomita 15 kila siku kutafuta maji, itakuwa historia mara tu bwawa litakapokamilika."

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, katiba ya Kenya inapaswa kurekebishwa ili kulipa baraza jipya la Seneti madaraka zaidi?

Angalia matokeo