Askari doria wa Kenya waua watuhumiwa watano wa ujangiri

Aprili 22, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Askari wa doria wa Kenya iliwauwa watuhumiwa watano wa ujangiri katika Wilaya ya West Pokot karibu na mpaka wa Uganda, Huduma za Wanyamapori ya Kenya (KWS) iliripoti hapo Jumamosi (tarehe 21 Aprili).

Majangiri walijeruhiwa katika mapambano ya silaha, yaliyoanza saa 7 usiku na kuendelea kwa zaidi ya dakika 40, KWS ilisema, na kuongeza kuwa katika eneo la tukio hilo, iliokoa kilo 50 za meno ya ndovu na bunduki tatu za mashambulizi.

Polisi wanamtafuta mtuhumiwa mmoja wa majangiri hao ambaye alitoroka, alisema meneja wa mawasiliano wa KWs Paul Udoto. "KWS inajitahidi zaidi kuliko zamani katika kumaliza vitendo vyote vya ujangiri na umiliki haramu wa bidhaa za wanyama pori," Udoto alisema, kwa mujibu wa Redio Capital FM News ya Kenya.

Majangia ni matatizo huko Kenya licha ya kuwepo sheria inayoikataza, na KWS inatoa adhabu kali kwa wanaoshiriki biashara haramu ya pembe za ndovu.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, katiba ya Kenya inapaswa kurekebishwa ili kulipa baraza jipya la Seneti madaraka zaidi?

Angalia matokeo