Mahakama kuu ya Kenya yatoa uamuzi kwa kuzingatia upatikanaji wa dawa za kijenasi za bei nafuu

Aprili 22, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Mahakama Kuu ya Kenya ilitoa uamuzi siku ya Ijumaa (tarehe 20 Aprili) kwamba tafsiri ya "ughushi" katika Sheria ya Kuzuia Ughushi ni pana mno na itaweza kuzuia upatikanaji wa dawa za kijenasi.

"Sheria haiko wazi na inaweza kupunguza upatikanaji wa dawa za kijenasi za bei nafuu, kwakuwa sheria imeshindwa kutofautisha kati ya ughushi na dawa za kijenasi," Jaji Mumbi Ngugi alisema wakati wa kutoa hukumu.

Mahakama Kuu ililiomba Bunge kupitia sheria ili kulinda dhidi ya utaifishaji wa dawa za kijenasi kwa kisingizio cha kukabiliana na dawa za kughushi. Hukumu pia ilieleza kwamba haki za kumiliki utaalamu hazipaswi kuzidi haki za kuishi na afya.

Mwishoni mwa mwaka jana, takriban watu milioni 1.6 nchini Kenya walikuwa wakiishi na VVU, kutokana na taarifa za shirika la UNAIDS, Programu ya Pamoja ya Umoja wa Mataifa kuhusu VVU/UKIMWI. Wakenya takriban 743,000 wanastahili kupata matibabu ya kupunguza makali, wakati 539,000 wanayapata.

"Watu wengi nchini Kenya wanazingatia dawa zenye ubora za kijenasi kwaajili ya maisha yao ya kila siku," alisema Mkurugenzi Mtendaji wa UNAIDS Michel Sidibé. "Uamuzi huu umeweka utaratibu wa kuhakikisha kwamba dawa za kuokoa maisha zinapatikana."

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, katiba ya Kenya inapaswa kurekebishwa ili kulipa baraza jipya la Seneti madaraka zaidi?

Angalia matokeo