Aprili 15, 2012
Kamanda mmoja wa al-Shabaab aliionya Sierra Leon hapo Jumapili (tarehe 15 Aprili) kutopeleka majeshi yake nchini Somalia, na kutishia kulipiza kisasi kwa askari wowote watakaoingia nchini humo, Radio ya Somalia ya RBC iliripoti.
Sheikh Abdirahman Muhumed Hudeyfa, kamanda wa al-Shabaab kusini ya Somalia, alitoa onyo hilo kupitia kituo cha radio cha al-Shabaab, kwa kudai kuwa majeshi ya wapinzani kutoka Sierra Leon ni ushahidi wa ushibdi unaodaiwa wa al-Shabaab kusini ya Somalia.
Al-Shabaab imekuwa katika shinikizo kubwa la operesheni za kijeshi kusini mwa Somalia, pàmoja na ripoti za za kuongezeka kwa migawanyiko katika kikundi na wanamgambo kukimbilia kaskazini kutoka maeneo yaliyokombolewa nan a majeshi ya AMISOM na serikali ya Somalia.
Sierra Leone imepangiwa kupeleka Somalia wanajeshi 850 hapo Juni kama sehemu ya Misheni ya Umoja wa Afrika nchini Somalia (AMISOM) inayofadhiliwa na Umoja wa Mataifa. Hivi karibuni, aafisa kutoka Sierra Leon walitembelea eneo la Gedo ncini Somalia kuchunguza maeneo ya nguvu ili kupeleka majeshi yatakayoshirikiana na Kenya, kituo cha radio kilitangaza.
Polisi nchini Tanzania walimkamata mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msingwa, na wafanyabiashara 60 k...
Mahakama moja ya Bosaso iliwatia hatiani na kuwapiga faini Wairani 78 siku ya Jumapili (tarehe 19...
Polisi nchini Tanzania waliwakamata watuhumiwa 15 kuhusiana na kulichoma Kanisa la Bethania kweny...
Mkuu wa Polisi wa Kenya, David Kimaiyo, ameondoa nafasi za afisa polisi wa jimbo, afisa wa upelel...
Watu wenye silaha waliwaua watu wawili na kuwajeruhi wengine wanne katika mashambulizi tofauti kw...
Mkutano wa kuzungumzia uwezekano wa uchimbaji mafuta na gesi, uwekezaji, usalama na miundombinu n...
Wizara ya Masuala ya Wanawake na Familia ya Puntland ilianza mafunzo ya siku nane hapo Juampili (...
Zaidi ya Wasomali milioni 1 hawatakuwa na "usalama wa chakula" hadi mwezi wa Septemba, Mtandao wa...
Ujumbe kutoka Jumuiya ya Maendeleo ya Pembe ya Afrika (IGAD) uliwatembelea maafisa mjini Mogadish...
Mshukiwa wa ugaidi na mke wake walipigwa risasi na kufa na maafisa sita wa polisi walijeruhiwa wa...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji
Maoni ya msomaji
Tunaviomba vikosi vyetu vya usalama kuvikamata hivi vijihalifu uchwara vya kukodiwa, lazima vipelekwe mbele ya sheria na kupatiwa adhabu ya haki kwa matendo yao ya uhalifu. Damu za watu wasio na hatia zilizomwagika zisipite bure. Kwa hivyo tunaomba hawa waletwe na washitakiwe ili uwe mfano na somo kwa wengine, kama vile Al-Shabaab na magenge yao ya kupangwa ambayo yanawalenga watu wa Somalia wasio na hatia. Vikosi vya usalama vya Somalia viendelee kuwasaka wahalifu hawa. Lazima wakamatwe ili kuiepusha jamii na uovu wao wa kigaidi.