Al-Shabaab wawaonua majeshi ya Sierra Leon wajiweke kando

Aprili 15, 2012

  • 1 Maoni
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Kamanda mmoja wa al-Shabaab aliionya Sierra Leon hapo Jumapili (tarehe 15 Aprili) kutopeleka majeshi yake nchini Somalia, na kutishia kulipiza kisasi kwa askari wowote watakaoingia nchini humo, Radio ya Somalia ya RBC iliripoti.

Sheikh Abdirahman Muhumed Hudeyfa, kamanda wa al-Shabaab kusini ya Somalia, alitoa onyo hilo kupitia kituo cha radio cha al-Shabaab, kwa kudai kuwa majeshi ya wapinzani kutoka Sierra Leon ni ushahidi wa ushibdi unaodaiwa wa al-Shabaab kusini ya Somalia.

Al-Shabaab imekuwa katika shinikizo kubwa la operesheni za kijeshi kusini mwa Somalia, pàmoja na ripoti za za kuongezeka kwa migawanyiko katika kikundi na wanamgambo kukimbilia kaskazini kutoka maeneo yaliyokombolewa nan a majeshi ya AMISOM na serikali ya Somalia.

Sierra Leone imepangiwa kupeleka Somalia wanajeshi 850 hapo Juni kama sehemu ya Misheni ya Umoja wa Afrika nchini Somalia (AMISOM) inayofadhiliwa na Umoja wa Mataifa. Hivi karibuni, aafisa kutoka Sierra Leon walitembelea eneo la Gedo ncini Somalia kuchunguza maeneo ya nguvu ili kupeleka majeshi yatakayoshirikiana na Kenya, kituo cha radio kilitangaza.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 1)

Dislike_icon(1)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Maoni ya msomaji

  • معاذ عبد الرحيم
    April 16, 2012 @ 01:23:56PM

    Tunaviomba vikosi vyetu vya usalama kuvikamata hivi vijihalifu uchwara vya kukodiwa, lazima vipelekwe mbele ya sheria na kupatiwa adhabu ya haki kwa matendo yao ya uhalifu. Damu za watu wasio na hatia zilizomwagika zisipite bure. Kwa hivyo tunaomba hawa waletwe na washitakiwe ili uwe mfano na somo kwa wengine, kama vile Al-Shabaab na magenge yao ya kupangwa ambayo yanawalenga watu wa Somalia wasio na hatia. Vikosi vya usalama vya Somalia viendelee kuwasaka wahalifu hawa. Lazima wakamatwe ili kuiepusha jamii na uovu wao wa kigaidi.

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo

Nyenzo