Mamlaka ya Viwanja vya ndege ya Kenya yafukuza wafanyakazi wanaogoma

Aprili 10, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Mamlaka ya Viwanja vya ndege ya Kenya (KAA) ilitangaza siku ya Jumatatu (tarehe 9 Aprili) kwamba imewafukuza wafanyakazi waliokaidi kurejea kazini kufuatia mgomo mwishoni mwa wiki, Redio Capital FM ya Kenya iliripoti.

"Wafanyakazi wote ambao bado wanajihusisha na mgomo usio halali wamechukuliwa kwamba hawajafika kazini na kwa kifupi wamefukuzwa," KAA ilieleza katika waraka wake.

KAA imesema kwamba zaidi ya asilimia 80 ya wafanyakazi wake 1,500 walioungana wamerejea kazini kufuatia mgomo mfupi ambao ulianza Ijumaa.

"Tunachukua fursa hii kuuhakikishia umma kwamba huduma katika viwanja vyetu vyote vya ndege zimeendelea bila vikwazo vyovyote," ulieleza waraka huo. Uongozi na wakala wa serikali walichukua hatua za dharula wakati wa mgomo, waraka ulieleza.

Nicholas Baraza, katibu wa Umoja wa Wafanyakazi wa Viwanja vya ndege na wafanyakazi mwega, alisema mgomo bado unaendelea. "Hadi labda tutakapokubaliana na KKA kuhusu mapato kwa kanuni ya kazi, hakuna jinsi ambayo wanachama wetu watarejea kazini," alisema.

Chama kilisema siku ya Jumatatu kwamba kitaendelea na wito wake kwa nyongeza ya malipo ya asilimia 25 kwa wafanyakazi.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo