Serikali ya Somalia yaongeza ushindi dhidi ya al-Shabaab

Aprili 10, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Serikali ya Somalia inaendelea kuikomboa nchi dhidi ya ugaidi na inaelekeza vita dhidi ya al-Shabaab katika “ngome zao nchini humo”, ilitangaza Serikali ya Mpito ya Shirikisho la Somalia hapo Jumatatu (tarehe 9 Aprili).

Katika taarifa rasmi, serikali hiyo imetaja mifano ya wilaya zilizokombolewa hivi karibuni za Bay, Bakol, Hiiraan na Galgadud kama sehemu za mkakati “kuuharibu uwezo wa al-Shabaab/al-Qaeda na kupunguza kitisho chake”.

Serikali ilitangaza kwamba inaelekea kwenye mkoa wa Bay, ikichukuwa hivi karibuni udhibiti wa Qansax-dheere, Burhakaba na Ufuroow.

Ili kudumisha amani na utulivu katika wilaya mpya zilizotekwa, vikosi vya serikali na vya Umoja wa Afrika wameweka vikosi vyao katika miji mikubwa na midogo “kutanua nguvu za serikali nje ya mji mkuu na kumaliza ugaidi wa al-Qaeda.”

Katika habari nyingine, maafisa wa kijeshi kutoka Sierra Leone waliomo kwenye kikosi cha Umoja wa Afrika waliwasili katika mkoa wa Gedo hapo Jumatatu, iliripoti Redio Mogadishu. Wanajeshi wa Sierra Leone wanatarajiwa kujiunga na AMISOM baada ya nwezi wa Juni.

Maofisa hao waliyatembelea maeneo ya vikosi vya usalama vya Somalia yaliyotawaliwa kutoka al-Shabaab hivi karibuni na kukutana na wawakilishi wa Serikali ya Somali Garbaharey kujadiliana mkakati wa kuwashinda al-Shabaab katika mkoa huo, alisema mbunge Mohamed Sayid Adam.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 2)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo

Nyenzo