Aprili 09, 2012
Waathirika wawili zaidi kutokana na shambulio la bomu la kujitoa muhanga katika Jumba la Maonesho la Taifa mjini Mogadishu siku ya Jumatano walikufa mwishoni mwa wiki kutokana na majeraha, wakiongeza idadi ya vifo kuwa sita, Mtandao wa Habari wa Garowe Online ya Somalia imeripoti Jumapili (tarehe 8 Aprili).
Mbunge Mowlid Ma'aney Mohamud na Faisal Haji Elmi, mshauri wa Waziri Mkuu Abdiweli Mohamed Ali, walifariki katika hospitali ya Aga Khan jijini Nairobi, ambako walihamishiwa kwa ajili ya matibabu baada ya kukaa katika Hospitali ya Medina ya Somalia.
Siku ya Jumapili, Ali alitoa taarifa ya rambirambi kwa familia za waathirika akiuita uvamizi kuwa ni mbaya, shirika la habari liliripoti. “Faisal alijitolea katika kuimarisha na kuendeleza serikali hii na Mungu atampeleka peponi,” taarifa hiyo ilisema.
Hali kadhalika, wabunge wametoa rambirambi zao kwa familia ya mwenzao aliyefariki, Mohamud, wakisema wamempoteza shujaa, Redio RBC ya Somalia iliripoti.
Raisi wa Kenya Uhuru Kenyatta siku ya Alhamisi (tarehe 23 Mei) alitoa majina mawili ya mwisho ya ...
Watu watano waliuawa na wanne kujeruhiwa katika mashambulizi mawili kwenye eneo la kaskazini mash...
Sababu kuu ya vurugu ambazo ziliua zaidi ya watu 150 katika Delta ya Mto Tana mwaka jana ilitokan...
Shirika la Afya Duniani (WHO) lilitangaza mlipuko wa polio katika Pembe ya Afrika siku ya Jumatan...
Majeshi ya serikali ya Somalia yamezifungia kampuni za mawasiliano ya simu na biashara nyingine h...
Serikali ya Somalia itaanza kuunda tawala za kikanda katika maeneo yaliyokombolewa kutoka kwa al-...
Waziri wa Nishati wa Djibouti Ali Yacoub Mohamoud na Balozi wa Japani nchini Djibouti Atsushi Nis...
Ufunguzi wa Mkutano wa Wasambazaji wa mafuta na gesi Tanzania utafanyika huko Dar es Salaam tareh...
Wabunge wameondoa hoja yao inayomtaka Waziri Mkuu Abdi Farah Shirdon na baraza lake la mawaziri k...
Rais Ahmed Silanyo wa mkoa wa Somaliland alikutana na Mwakilishi Maalum wa Umoja wa Ulaya kwa Som...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji