Kibaki ataka kuimarishwa kwa sheria kwa wafanyabiashara

Aprili 05, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Rais wa Kenya, Mwai Kibaki, hapo Jumatano (Aprili 4) aliitaka serikali kuweka sheria ndogo ndogo za kusaidia kuwainua wafanyabiashara wadogo wadogo, liliripoti gazeti la nchi hiyo la Daily Nation.

Taasisi za umma lazima zishirikiane kuinua maisha ya wananachi, alisema Rais Kibaki katika uzinduzi wa soko jipya la Kamukunji huko Nyeri. Soko hilo lililojengwa na serikali kwa gharama ya shilingi milioni 223 (dola milioni 2.6 za Kimarekani), lina maduka 500 kwa wafanyabiashara wadogo wadogo, mkahawa na sehemu ya huduma.

Soko hilo lilijengwa kufuatia ushirikiano wa Wizara ya Nyumba, Mpango wa Kupandisha Daraja Maeneo ya Mabanda na Baraza la Manispaa la Nyeri.

Kibaki alisema soko hilo jipya litakuwa kama kiunganisho baina ya uzalishaji wa soko na uinuaji wa uchumi wa Nyeri. Soko hilo litawaondoa wafanyabiashara wanaorandisha bidhaa zao mitaani na kuwaweka pamoja na hivyo kutoa mazingira ya kufanya kazi pamoja, alisema Rais Kibaki.

Kibaki aliyataka mashirika ya serikali kuiga ushirikiano kama huu ili kuinua utoaji wa huduma muhimu kwa wananchi. Alisema mageuzi kama hayo yanahakikisha kuwa maeneo ya vijijini yanapata ukuwaji wa uchumi na hivyo kuwavutia wawekezaji, na matokeo yake kuibadilisha sekta ya kilimo ya Kenya kutoka ile inayotegemea mazao ya chakula kwenda ile inayotilia mkazo biashara.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo

Nyenzo