Aprili 05, 2012
Waziri Mkuu wa Somalia Abdiweli Mohamed Ali alisema shambulizi katika Jumba la Maonesho la Taifa hapo Jumatano (tarehe 4 Aprili) hakutorejesha nyuma juhudi za serikali za kupambana na al-Shabaab, gazeti la mtandaoni la Somalia la Garowe Online liliripoti.
"Hii haitapunguza wala kuturejesha nyuma kutoka njia yetu," Ali alisema katika mkutano na waandishi wa habari mjini Mogadishu saa chache baada ya mlipuko. Al-Shabaab wanakabiliwa na kushindwa, na ndio maana wanajikaza katika kudhoofisha na kutumia mbinu chafu kama hizi."
Kiasi cha watu sita waliuwawa na 10 kujeruhiwa wakati mwanamke mwenye umri mdogo aliporipotiwa kujitoa muhanga kwa kuvaa mkanda wenye mabomu, ambaye alimleng Ali na Viongozi wengine wakati wa maadhimisho ya mwaka mmoja wa kituo cha televisheni ya Taifa.
"Wananchi wasio na hatia waliuawa katika mlipuko huo na serikali ya TFG inashughulikia kuboresha usalama wetu ili mashambulio kama haya yasitokee ten," alisema Ali, huku akiwashukuru viongozi wa usalama, wanajeshi na mapolisi kwa kufanikisha uzuiaji wa mashambulio mengine kama hili huko Mogadishu mara kadhaa.
Majeshi ya Usalama yapo katika hadhari ya hali ya juu jijini, kaimu mkuu wa usalama wa Mkoa wa Banaadir, Warsame Mohammed Jodah, aliiambia Shabelle ya Somalia siku ya Jumatano.
Mogadishu imekuwa ikikabiliwa na mashambulio ya mauaji na makombora tangia al-Qaeda-iwashirikishe katika matukio ya al-Shabaab yaliyotelekezwa katika makambi ya kudumu ya al-Shabaab katika mji mwezi Agosti na kurejea kwa mbinu za mapigano ya msituni.
Waziri mkuu alituma salamu zake za rambirambi kwa familia za wale waliouawa katika mlipuko ikiwa ni pamoja na rais wa Kamati ya Olimpiki ya Somalia Adaan Haaji Yabaroow "Wiish" na kiongozi mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu la Somalia Said Mohamed Nur "Mugaanbe".
Baadhi ya wabunge wa Somalia wameitupilia mbali hoja ya kumtaka waziri mkuu na baraza lake la maw...
Wabunge wa upinzani walidai kwamba serikali ya Tanzania imekuwa ikibana uhuru wa kujieleza na kud...
Sampuli ya DNA iliyochukuliwa kwenye mswaki uliokuwemo kwenye begi lililokuwa na risasi lililopat...
Wakenya kumi na wasaba wameshtakiwa kwa kuvunja amani, kufanya ghasia na ukatili dhidi ya wanyama...
Al-Shabaab imedai kuhusika na urushwaji wa makombora kwenye kasri ya rais mjini Mogadishu siku ya...
Wanajeshi wa Uganda wa Kikosi Namba 9+ wanarudi nyumbani baada ya kukamilisha miezi 13 ya ziara y...
Kikosi cha polisi cha Kenya kitaanza uhakiki wa kina wa maofisa mwezi ujao, kikianza na kusaili w...
Ujambazi ulizuiwa katika ofisi za usalama za Wells Fargo huko Mombasa ulisababisha kifo cha watu ...
Rais wa Ghana John Dramani Mahama aliahidi msaada wa nchi yake katika kipindi cha ujenzi mpya wa ...
Polisi nchini Tanzania walimkamata mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msingwa, na wafanyabiashara 60 k...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji