Aprili 03, 2012
Al-Shabaab Jumanne asubuhi (tarehe 3 Aprili) walishambulia kwa kuvizia malori kutoka Kamati ya Kimataifa ya Shirika la Msalaba Mwekundu (ICRC) ambayo yalikuwa yamebeba msaada wa chakula kwa mkoa wa Gedo, Serikali ya Mpito ya Sirikisho ya Somalia (TGF) ilisema.
Msemaji wa jeshi la TFG Aden Ahmed Hirse alisema msafara huo wa malori yaliyokodiwa na ICRC yalishambuliwa katika barabara inayounganisha wilaya za Elwak na El-Adde, kwa mujibu wa Mtandao wa Habari wa Shabelle wa Somalia.
Hirse alisema dereva wa Kisomali aliuawa katika shambulio hilo. Vikosi vya TFG vilifika katika eneo la tukio na kufanya operesheni ya ukaguzi kuwasaka washambuliaji, alisema.
Ofisa wa ICRC alisema msaada wa kibinadamu wa chakula ulikusudiwa kwa familia za Kisomali zilizoathirika na ukame huko magharibi kusini mwa Somalia.
Polisi waliwakamata mamia ya watu wanaoshukiwa kuwa wapiganaji wa al-Shabaab katika wilaya za Hod...
Kongamano la siku tatu juu ya elimu lilifunguliwa mjini Mogadishu siku ya Jumanne (tarehe 18 Juni...
Wanajeshi wa serikali ya Somalia wakisaidiwa na wanajeshi wa Misheni wa Umoja wa Mataifa (AMISOM)...
Waziri wa Mambo ya Ndani na Uratibu wa Serikali ya Kitaifa, Joseph Ole Lenku, siku ya Jumatatu (t...
Moto kwenye soko kubwa la Garissa uliharibu zaidi ya maduka 100 usiku wa Jumatatu (tarehe 17 Juni...
Waziri wa Umoja wa Kitaifa wa Djibouti Zahra Youssouf Kayad alisaini mikataba ya miradi miwili ye...
Kamati ya bajeti ya Bunge ya Kenya imekataa pendekezo la kununua ofisi mpya kwa aliyekuwa Rais Mw...
Moto ulifanya uharibifu mkubwa katika mji wa Balbala huko Djibouti siku ya Jumapili (tarehe 16 Ju...
Picha ambazo al-Shabaab ilizituma siku za Jumapili (tarehe 16 Juni) kwenye mtandao wa Twitter za ...
Polisi nchini Kenya walimuua mtuhumiwa wa ugaidi, Kassim Omolo Otemo, mjini Mombasa wakati uvamiz...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji